Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 14:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 14:5
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa muda wa miaka kumi na miwili walikuwa wakimutii mufalme Kedorilaomeri, lakini katika mwaka wa kumi na tatu, wakamwasi.


Kisha, mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu waliteremuka wakati wa mavuno, wakamufikia Daudi kwenye pango kule Adulamu. Wakati ule kundi la waaskari wa Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.


Wafilistini walifika na kujitawanya kwenye Bonde la Refaimu.


Kwa mara ya pili, Wafilistini walifika tena na kujitawanya kwenye bonde la Refaimu.


Kisha mashujaa watatu kati ya wakubwa makumi tatu wakamwendea Daudi kwenye mulima wa pango la Adulamu. Wakati ule jeshi la Wafilistini lilikuwa limepiga kambi katika bonde la Refaimu.


Wafilistini wakafika wakaanza mashambulizi katika bonde la Refaimu.


Kule, walipata malisho tele, tena mazuri sana na tena inchi ilikuwa wazi, tulivu na yenye amani, maana wenyeji wa inchi hiyo wa zamani walikuwa wazao wa Hamu.


Halafu Israeli akaingia katika inchi ya Misri; Yakobo akakuwa mugeni katika inchi ya Hamu.


Wakafanya maajabu ya Mungu kati ya Wamisri, na miujiza katika inchi hiyo ya Hamu.


maajabu katika inchi hiyo ya Hamu, na mambo ya kutisha katika bahari Nyekundu.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri; ndilo chipukizi la kwanza katika kambi la Hamu.


Itakuwa kama wakati wa mavuno, wakati wamekwisha kuokota ngano, na kukusanya masuke katika mukono. Hakika, itakuwa kama bonde la Refaimu wakati wamekwisha kuvuna ngano.


Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;


Kabila la Gadi likajenga miji ya Hesiboni, Eleale, Kiriataimu,


Alifanya hivyo kisha Yawe kumushinda mufalme Sihoni wa Waamori ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Hesiboni, na mufalme Ogi wa Basani ambaye alikuwa anakaa katika muji wa Astaroti na Edirei.


(Mufalme Ogi ndiye peke yake aliyebakia kati ya Warefai. Kitanda chake kilichotengenezwa kwa chuma, kilikuwa na urefu wa metre ine na upana wa karibu metre mbili. Kitanda hicho kipo katika muji wa Waamori wa Raba.)


Kisha nikalipatia nusu ya lile kabila la Manase sehemu iliyobaki ya Gileadi pamoja na Basani yote iliyotawaliwa na Ogi, ni kusema eneo lote la Argobu. Inchi yote ya Basani ilijulikana kama vile inchi ya Warefai.


Muwasaidie wandugu zenu Waisraeli mpaka Yawe atakapowajalia watulie pahali pao kama vile nanyi mulivyotulia, ni kusema nao vilevile warizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapatia huko ngambo ya Yordani. Nyuma ya hayo, mutaweza kurudia katika inchi yenu hii ambayo nimewapa ikuwe yenu!’


Musiwaogope maana Yawe, Mungu wenu, ndiye atakayepigana kwa ajili yenu.’


Mwingine ni mufalme Ogi mumoja wa Warefaimu waliobaki, ambaye alitawala Basani na alikaa Asitaroti au Edirei.


na ufalme wote wa Ogi mumoja wa Warefaimu waliobaki, ambaye alitawala kule Asitaroti na Edirei katika Basani. Musa alikuwa amewashinda hao wote na kuwafukuzia mbali.


Kiriataimu, Sibuma, Zereti-Sahari, kule kwa kilima katika bonde,


nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.


Tumesikia yote aliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ngambo ya muto Yordani, mufalme Sihoni wa Hesiboni na mufalme Ogi wa Basani aliyekaa kule Astaroti.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ