Gehazi, mutumishi wa Elisha mutu wa Mungu, akasema: “Bwana wangu amemwachilia Namani wa Aramu aende bila kupokea chochote alicholeta. Kama vile Yawe anavyoishi, nitamufuata kusudi nipate kitu kutoka kwake.”
Sasa mimi niko tayari kufika kwenu kwa mara ya tatu, nami sitawalemea. Maana sihitaji mali yenu, lakini ninawahitaji ninyi. Kwa sababu si kazi ya watoto kuwawekea wazazi wao akiba, lakini ni kazi ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba.
Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”