Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 14:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 14:20
30 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mufalme wa Sodoma akamwambia Abramu: “Unipe wale watu, lakini ujitwalie mali yote wewe mwenyewe.”


akisema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Yawe ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja mpaka kwa jamaa ya bwana wangu!”


Nalo jiwe hili nililosimika hapa kama nguzo, litakuwa nyumba yako Mungu, nami nitakupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”


Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”


Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo katika inchi ya Misri. Kila mwanainchi anapaswa kutoa sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa mufalme. Udongo wa makuhani tu ndio haukununuliwa na kufanywa mali ya mufalme.


Tena akasema: “Semu abarikiwe na Yawe, Mungu wangu! Kanana akuwe mutumwa wake.


Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”


na mule ndani wakaweka matoleo, sehemu moja za kumi na vyote vilivyotakaswa kwa uaminifu. Wakamuweka Konania, Mulawi, kuwa musimamizi mukubwa muchungaji wa vitu hivyo, na ndugu yake, Simea kuwa musaidizi wake.


Kwa kufuata vile ilivyoandikwa katika Sheria kila muzaliwa wa kwanza wa kiume kati ya wana wetu, katika nyumba zetu, atapelekwa katika nyumba ya Mungu wetu kwa makuhani wanaotumika mule, vilevile tutapeleka kila muzaliwa wa kwanza dume wa ngombe zetu, mbuzi zetu na kondoo zetu.


Kisha, watu wote wa Israeli, wakaanza tena kuleta zaka zao za unga, divai na mafuta kwenye gala.


Zaburi ya Daudi. Atukuzwe Yawe, yeye ni: nguvu yangu, yule anayeizoeza mikono yangu kupigana vita na kuvifundisha vidole vyangu kugombana,


Kwa mukono wako mwenyewe uliyafukuza mataifa, na mahali pao ukawaikalisha watu wako; uliyaazibu mataifa, na kuwafanikisha watu wako.


Anapanda juu akichukua wafungwa, anapokea zawadi kutoka kwa watu, hata kutoka kwa watu walioasi, Yawe apate kukaa huko.


Yetro akasema: “Atukuzwe Yawe ambaye amewaokoa toka katika mikono ya Wamisri na kutoka katika mukono wa mufalme wa Misri.


Enyi Waisraeli, muende basi kule Beteli na kuniasi! Muende Gilgali muongeze makosa yenu! Mutoe sadaka zenu kila asubui na zaka zenu kwa siku ya tatu.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Ninawajibia hivi: Ni sawa kwa mutu kumudanganya Mungu? Hapana! Lakini ninyi munanidanganya! Ingawa hivyo ninyi munauliza: Tunakudanganya kwa namna gani? Kweli! Munanidanganya juu ya zaka na sadaka zenu.


Katika siku ya kwanza ya sikukuu ya majuma wakati munapomutolea Yawe malimbuko ya ngano zenu, mutafanya mukutano mutakatifu; musifanye kazi.


Ninafunga kula chakula mara mbili kila juma na ninatoa fungu moja la kumi la vitu vyote ninavyopata.’


kuwa mutumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa mengine. Ninafanya kazi ya ukuhani ya kuhubiri Habari Njema ya Mungu, kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuwa kama sadaka inayokubaliwa na Mungu na iliyotakaswa na Roho Mutakatifu.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Musikule vitu hivi pahali munapoishi: sehemu ya kumi za ngano zenu, divai zenu au mafuta yenu, wazaliwa wa kwanza wa ngombe wenu au kondoo wenu, au sadaka zenu za kutimiza kiapo au za mapenzi, au matoleo mengine.


Halafu muende pahali ambapo Yawe, Mungu wenu amepachagua kwa kuweka jina lake, na mukiwa mbele yake mutakula sehemu ya kumi ya ngano yenu, ya divai yenu na ya mafuta, na ya wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu. Mufanye hivi kusudi mujifunze kumwogopa Yawe, Mungu wenu siku zote.


Kila mwisho wa mwaka wa tatu mutoe sehemu ya kumi ya mazao yenu yote na kuyaweka akiba katika miji yenu.


Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ