Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 14:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 14:19
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abramu akamwambia mufalme wa Sodoma: “Ninaapa kwa Yawe, Mungu Mukubwa, aliyeumba mbingu na dunia,


nami nitakuapisha kwa jina la Yawe, Mungu wa mbingu na dunia, kwamba hautamwoea mwana wangu binti yeyote kati ya wabinti za Wakanana ninaoishi nao.


Halafu unitengenezee chakula kitamu, kile ninachopenda, uniletee nikule, nipate kukubariki mbele ya kufa kwangu.”


Kisha Yakobo akamubariki mufalme, akaondoka.


Kisha, Yosefu akamuleta baba yake Yakobo kumwamukia mufalme. Naye Yakobo akamupa mufalme baraka zake.


Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno baba yao aliyowaambia alipowabariki, kila mumoja wao kama alivyostahili.


aliwatuma watu kule Yabesi-Gileadi na ujumbe: “Yawe awabariki kwa maana mulitendea bwana wenu Saulo mema kwa kumuzika.


Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Mufalme Hezekia na wakubwa wake walipokuja kuangalia mafungu yale, wakamushukuru Yawe na watu wake wa Israeli.


Mubarikiwe na Yawe, aliyeumba mbingu na dunia.


Mbingu ni mali ya Yawe, lakini amewapa wanadamu dunia.


Zaburi ya Daudi. Dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake ni vya Yawe; ulimwengu na wote wanaoishi ndani yake ni mali yake.


maana nyama wote wa pori ni mali yangu, na maelfu ya nyama wa milima ni wangu.


Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Kisha akawakumbatia watoto wale, akaweka mikono juu yao na kuwabariki.


Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Mwanamuke yule akaendelea kumufuata Paulo na sisi, akilalamika akisema: “Watu hawa ni watumishi wa Mungu Mukubwa. Wanawatangazia ninyi namna gani munavyoweza kuokolewa.”


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Basi tumusifu Mungu kwa sababu ya utukufu wa neema yake aliyotujalia kwa njia ya Mwana wake mupendwa.


Angalia, mbingu hata mbingu za mbingu ni mali ya Yawe, Mungu wenu, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake.


Boazi akasema: “Yawe akubariki, kwa maana kwa yote unayofanya unaonyesha heshima zaidi kuliko uliyoyafanya pale mbele, kwa maana haukuwatafuta vijana wamasikini au tajiri wakuoe.


Samweli alipomufikia Saulo, Saulo akamwambia Samweli: “Yawe akubariki! Nimetimiza amri ya Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ