Mwanzo 14:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
17 Abramu aliporudi kisha kumushinda mufalme Kedorilaomeri na wenzake, mufalme wa Sodoma akatoka na kwenda kukutana naye katika bonde la Sawe ni kusema bonde la Mufalme.
Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.
Katika mwaka wa kumi na ine, mufalme Kedorilaomeri na wale wafalme wenzake wakakuja na kuwashinda watu wa Refaimu kule Astaroti-Karnaimu, Wazuzi kule Hamu, Waemi kule Sawe-Kiriataimu,
Abusaloma, alipokuwa angali anaishi, alikuwa amejijengea na kujisimikia nguzo inayokuwa kwenye Bonde la Mufalme, maana alisema: “Mimi sina mutoto mwanaume wa kudumisha jina langu kusudi nikumbukwe.” Nguzo hiyo aliipa jina lake, na inaitwa “Nguzo ya Abusaloma” mpaka leo.
Huyu Melkisedeki alikuwa mufalme wa Salemu na kuhani wa Mungu Mukubwa. Abrahamu alipokuwa akirudi toka katika vita nyuma ya kuwashinda wafalme wane, Melkisedeki alikutana naye na kumubariki,
Yefuta alipokuwa anarudi kwake kule Misipa, binti yake akatoka kuja kumupokea akicheza na kupiga matari. Binti huyo alikuwa ndiye mutoto wake wa pekee. Yefuta hakukuwa na mutoto mwingine mwanaume wala mwanamuke.
Waaskari walipokuwa wanarudi kwenye nyumba, pamoja na Daudi kisha kumwua yule Mufilistini, wanawake kutoka kila muji katika Israeli walitoka kwenda kumupokea mufalme Saulo. Wanawake nao walikuwa wanaimba nyimbo za furaha, wakipiga matari na vinubi.