Abramu alipopata habari kwamba mwipwa wake amekamatwa kuwa mufungwa, akatoka na watu wake mashujaa mia tatu na kumi na wanane waliozaliwa katika nyumba yake, akawafuatilia waadui mpaka Dani.
Basi, Yosefu akaondoka kwenda kumuzika baba yake akisindikizwa na watumishi wengi wa mufalme wa Misri, wazee wa nyumba ya mufalme, pamoja na wazee wa inchi nzima ya Misri.
Ni nani aliyemwita shujaa toka mashariki, mutu ambaye anapata ushindi popote anapoenda? Mimi ninayaweka mataifa katika mikono yake, naye anawaponda wafalme chini ya miguu yake! Upanga wake unawafanya kuwa kama mavumbi, kwa upinde wake anawapeperusha kama maganda.