Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 14:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 14:13
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na vilevile babu ya Wayebusi, Waamori, Wagirgasi,


Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Basi, sitatwaa kitu chochote isipokuwa tu vile vitu ambayo vijana wangu walikula na sehemu ya wale waliokuwa pamoja nami – Aneri, Eskoli na Mamure – ambao wana haki nayo.”


Yawe alimutokea Abrahamu kwenye miti ya mielo ya Mamure. Abrahamu alikuwa anaikaa kwenye mulango wa hema yake wakati wa joto la muchana.


Basi, Abrahamu akatwaa kondoo na ngombe akamupa Abimeleki nao wawili wakafanya agano kati yao.


Hivyo, wakafanya agano kule Beri-Seba. Abimeleki na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akaondoka na kurudi katika inchi ya Wafilistini.


akaita watumishi wa nyumba yake na kuwaambia: “Huyu Mwebrania tuliyeletewa anatuzarau. Alikuja kwangu akitaka kunishika kwa nguvu, lakini nikapiga kelele.


Maana mimi nilitoroshwa kutoka inchi ya Waebrania na hapa Misri sijafanya kitu chochote kinachostahili nitiwe katika kifungo.”


Basi, kijana mumoja Mwebrania, mutumishi wa jemadari wa waaskari walinzi, alikuwa pamoja nasi katika kifungo. Tulipomwelezea ndoto zetu, yeye aliweza kutuelezea kila mumoja wetu kulingana na ndoto yake.


Yosefu alitayarishiwa chakula chake peke yake, na wandugu zake wakatayarishiwa peke yao. Vilevile Wamisri waliokula pamoja naye, wakatayarishiwa peke yao, maana ni chukizo kwa Wamisri kula chakula pamoja na Waebrania.


Basi Wasabea wakatushambulia na kunyanganya nyama na kuua watumishi kwa upanga. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.


Alipokifungua, akamwona yule mutoto muchanga akilia. Basi, akamwonea huruma, akasema: “Huyu ni mumoja wa watoto wa Waebrania.”


“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’


watumwa na wajakazi wao wa Kiebrania, kusudi mutu yeyote asimufanye Muyuda mwenzake kuwa mutumwa.


Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.


Walipofika katika Bonde la Eskoli, watu hao wakakata shada la muzabibu lililokuwa na matunda mengi nalo lilibebwa na watu wawili juu ya muti. Wakatwaa vilevile makomamanga na tini.


Waisraeli wakamupelekea mufalme Sihoni wa Waamori, ujumbe huu:


Watu wale ni Waebrania? Mimi vilevile. Wao ni Waisraeli? Mimi vilevile. Wao ni wa uzao wa Abrahamu? Mimi vilevile.


Ndani yenu mukuwe na nia kama hii iliyokuwa ndani ya Kristo Yesu:


Wakubwa wa waaskari wa Wafilistini waliuliza: “Waebrania hawa wanafanya nini hapa?” Akisi akawajibu wale wakubwa wa Wafilistini: “Huyu ni Daudi, mutumishi wa Saulo mufalme wa Israeli; naye amekuwa nami kwa miaka fulani. Na tangu alipokimbilia kwangu, sijamupata na kosa lolote.”


Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ