Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Angalia inchi hii yote mbele yako. Na tutengane. Ukikwenda kushoto, mimi nitakwenda kuume. Ukikwenda kuume, mimi nitakwenda kushoto.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 13:9
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).


Basi, Abramu akamwambia Loti: “Kusikuwe ugomvi kati yetu wala kati ya wachungaji wako na wachungaji wangu, kwa sababu sisi ni jamaa moja.


Tena Abimeleki akamwambia Abrahamu: “Angalia, inchi hii yote ni yangu! Basi, chagua popote unapopenda, ukae.”


Kwa hiyo mutaishi pamoja nasi; mutakuwa huru katika inchi hii. Mutaishi humu, mufanye biashara na kujipatia mali.”


Ninaposema kwamba ninataka amani, wao wanataka tu vita.


Basi! Leo ninafungua minyororo toka mikono yako. Kama unaona ni vizuri kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi tuende pamoja; mimi nitakutunza vizuri. Lakini kama unaona si vizuri kwako kwenda pamoja nami mpaka Babeli, basi, usikuje. Ujue kwamba unaweza kwenda popote katika inchi hii. Basi kwenda kwenye unaona ni vizuri kwenda.


Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, muishi katika amani na watu wote.


Kweli mambo haya ya kuwa na mashitaki kati yenu yanahakikisha kwamba mumeshindwa kabisa. Si ingekuwa vizuri zaidi kwenu kuvumilia ubaya? Si ingekuwa vizuri zaidi kunyanganywa mali zenu?


Mujikaze kwa kuishi katika amani na watu wote na kuishi katika utakatifu, kwa sababu hakuna mutu asiyeishi katika hali hiyo atakayemwona Bwana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ