Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.
Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.
Baba yake akamwambia: “Kwenda uwaangalie wandugu zako na nyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamutuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Sekemu,
Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.
Nyuma ya mambo yale, Daudi alimwomba Yawe shauri, akasema: “Niende kwenye muji mumoja kati ya miji ya Yuda?” Yawe akamwambia: “Kwenda!” Daudi akamwuliza: “Niende katika muji gani?” Yawe akamujibu: “Kwenda kwenye muji wa Hebroni.”
Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.
Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya inchi ya Yuda kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriati-Arba au muji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Muji huo sasa unaitwa Hebroni.