Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 13:16
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”


Zaidi ya hayo, malaika wa Yawe akamwambia Hagari: “Nitawazidisha wazao wako hata wasiweze kuhesabika kwa wingi wao.”


Nitamubariki, naye atakuzalia mutoto mwanaume. Nitamubariki Sara, naye atakuwa mama wa mataifa mengi na wafalme wa mataifa watatoka kwake.”


Nami nitafanya agano nawe na kuwazidisha wazao wako.”


“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.


Nitakufanya ukuwe na wazao wengi sana. Toka kwako nitatokeza mataifa mengi na wafalme.


Yeye atakuwa baba wa taifa kubwa na kwa njia yake mataifa yote ya ulimwengu yatabarikiwa!


Na juu ya huyo mwana wa mujakazi wako nitamufanya akuwe baba wa taifa kubwa kwa sababu yeye vilevile ni mutoto wako.”


hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Ninakuomba uniokoe sasa kutoka kwa ndugu yangu Esau, maana nina hofu kwamba atatushambulia na kutuua wote, mama pamoja na watoto.


Wewe uliniahidi kunitendea mema na kuwafanya wazao wangu wakuwe wengi kama muchanga wa bahari ambao hauhesabiki kwa wingi wake.”


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.


Na hapa umeniweka kati ya watu wako ambao umewachagua; nao ni wengi hata hawawezi kuhesabika kwa sababu ya wingi wao.


Watu wa Yuda na wa Israeli walikuwa wengi kama muchanga wa bahari, nao walikuwa wakikula, wakikunywa, na kufurahi.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


Yoabu akamupelekea mufalme Daudi hesabu ya watu: katika inchi yote wa Israeli kulikuwa wanaume milioni moja na elfu mia moja, wenye ujuzi wa kutumia mapanga, na katika inchi ya Yuda kulikuwa watu elfu mia ine na makumi saba wenye kutumia mapanga.


Mufalme Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa chini ya umri wa miaka makumi mbili kwa maana Yawe aliahidi kuwaongeza Waisraeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.


Sasa, ee Mungu, Yawe, utimize ahadi uliyomupa Daudi baba yangu. Umeniweka kuwa mufalme juu ya watu hawa wanaokuwa wengi kama mavumbi.


Utaona vilevile wazao wako watakuwa wengi, wengi kama majani katika mashamba.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.


Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.


Nani anayeweza kuhesabu wingi wa watu wa Yakobo, au kuhesabu makundi ya Waisraeli? Nikufe kifo cha haki, mwisho wangu ukuwe kama wao.


Yawe, Mungu wenu, amewafanya mukuwe wengi; leo mumekuwa wengi kama vile nyota za mbinguni.


Kwa sababu hiyo, kwa njia ya mutu mumoja aliyekuwa akingojea kufa, kukazaliwa wazao wengi sana kama nyota na kama muchanga unaokuwa kandokando ya bahari.


Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.


Kila mara Waisraeli walipopanda mbegu katika mashamba, Wamidiani, Waamaleki na watu wengine wa kule upande wa mashariki walikuja kuwashambulia.


Waadui waliozoea kuja kwa wingi kama nzige, pamoja na ngombe na ngamia wao na kufanya makao yao katika inchi ya Israeli, waliharibu inchi ya Israeli kwa vile walikuwa wengi sana wasiohesabika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ