Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 13:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Inchi hii yote unayoona nitakupa wewe na wazao wako ikuwe yenu milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 13:15
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Basi, simama uitembelee inchi hii katika upana na urefu, maana nitakupa wewe inchi ile.”


Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Yawe akamwambia Abramu: “Mimi ni Yawe niliyekuleta toka Uri, muji wa Wakaldea, kusudi nikupe inchi hii uirizi.”


Yeye atakuwa baba wa taifa kubwa na kwa njia yake mataifa yote ya ulimwengu yatabarikiwa!


Yawe, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika inchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazao wangu inchi hii. Yeye atamutuma malaika wake mbele yako kusudi umuletee mwana wangu muke kutoka kule.


Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Akubariki wewe pamoja na wazao wako kama alivyomubariki Abrahamu, upate kurizi inchi ambamo unakaa kama mugeni, inchi ambayo Mungu alimupa Abrahamu!”


Inchi niliyowapa Abrahamu na Isaka nitakupa wewe na wazao wako.”


Akaniambia: ‘Nitakufanya ukuwe na wazao na uongezeke. Nitakufanya ukuwe babu ya jamii kubwa za watu. Inchi hii nitawapa wazao wako, wairizi milele.’ ”


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Alisema: “Nitawapa inchi ya Kanana, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”


Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?


Waliobarikiwa na Yawe watarizi inchi, lakini waliolaaniwa naye wataongolewa.


Watu wa haki watarizi inchi, nao wataishi humo milele.


Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.


Yawe akamwambia Musa: Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa katika inchi ya Misri. Muende katika inchi niliyowapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema: Nitawapa wazao wenu inchi hii.


Sisi watakatifu wako tulirizi inchi kwa muda kidogo tu, lakini waadui zetu wakakuja wakaharibu hekalu lako.


Uwaamuru Waisraeli ukisema: Mutakapoingia Kanana, inchi ambayo ninawapa ikuwe inchi yenu, mipaka ya eneo lenu lote itakuwa kama hivi.


Heri wale wanaokuwa wapole, maana watarizi dunia!


Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”


Munaweza kuirizi inchi yao si kwa sababu ninyi ni watu wa haki wenye mioyo ya usawa; lakini Yawe, Mungu wenu, anawafukuza watu hao mbele yenu kwa sababu ni waovu na anataka kuweka imara lile neno alilowaapia babu zenu, Abrahamu, Isaka na Yakobo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ