Mwanzo 13:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
14 Nyuma ya Loti kujitenga na Abramu, Yawe akamwambia Abramu: “Inua macho yako toka pale unapokuwa, utazame pande zote: kaskazini, kusini, mashariki na magaribi.
Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).
Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.
Inua macho uangalie pande zote; watu wako wote wanakusanyika na kukufikia. Kama vile ninavyoishi, watu wako watakuwa kwako kama mapambo, utawafurahia kama vile bibi arusi anavyofanya na taji lake. –Ni ujumbe wa Yawe.
Panda mpaka kwenye kilele cha mulima Pisiga, uangalie vizuri upande wa magaribi, kaskazini, kusini na mashariki, na kuiona inchi hiyo; lakini wewe hautavuka huu muto Yordani.
Basi, Musa akaondoka kwenye bonde la Moabu, akaenda kwenye mulima Nebo, akapanda juu ya kilele cha Pisiga kinachoelekeana na Yeriko. Hapo Yawe akamwonyesha inchi yote: toka Gileadi mpaka Dani,