Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).
Nyuma ya Loti kujitenga na Abramu, Yawe akamwambia Abramu: “Inua macho yako toka pale unapokuwa, utazame pande zote: kaskazini, kusini, mashariki na magaribi.
Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”
Usisahau warafiki zako wala wa baba yako. Ukipatwa na magumu usikimbilie kwa ndugu yako. Afazali jirani ambaye iko karibu kuliko ndugu anayekuwa mbali.
Upande wa mashariki, mupaka utakuwa muto Yordani unaoelekea kati ya Haurani na Damasiki, Gileadi na inchi ya Israeli. Vilevile mupaka utapitia upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi mpaka Tamari.
Tusiache kukusanyika pamoja, kama vile wamoja wanavyozoea kufanya. Lakini tuonyane, na zaidi sana kufuatana na vile munavyoona kwamba Siku ya Bwana inakaribia.