Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 13:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Loti akainua macho yake, akaona bonde la muto Yordani, akaona kwamba lina maji ya kutosha kila pahali, kama vile bustani ya Yawe na kama vile inchi ya Misri upande wa Soari. (Hii ilikuwa mbele Yawe hajaiangamiza miji ya Sodoma na Gomora).

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 13:10
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hawa ndio wazao wa Tera, baba ya Abramu, Nahori na Harani. Harani alikuwa baba ya Loti.


Kwa hiyo, Loti akajichagulia bonde lote la muto Yordani, akaelekea upande wa mashariki, na hivyo wakatengana.


Angalia inchi hii yote mbele yako. Na tutengane. Ukikwenda kushoto, mimi nitakwenda kuume. Ukikwenda kuume, mimi nitakwenda kushoto.”


wakapigana vita na Bera mufalme wa Sodoma, na Birsa mufalme wa Gomora, Sinabu mufalme wa Adima, Semeberi mufalme wa Seboimu, na mufalme wa Bela ni kusema Soari.


Halafu mufalme wa Sodoma, mufalme wa Gomora, mufalme wa Adima, mufalme wa Seboimu na mufalme wa Bela


Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


Inchi yote ya Misri iko chini yako; uwape baba yako na wandugu zako sehemu bora ya inchi hii. Uwaache wakae katika eneo la Goseni. Na ikiwa unawafahamu watu mashujaa kati yao, uwachague wakuwe waangalizi wa nyama wangu.”


wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.


Vitu hivyo vyote mufalme alivitengeneza katika kiwanda cha Yordani, sehemu ya udongo wa mufinyanzi iliyokuwa kati ya Sukoti na Zaretani.


Muto ukifurika haogopi, hatishiki hata muto Yordani ukifurikia katika kinywa.


Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.


Mimi Yawe nitaufariji Sayuni, nitatengeneza pahali pake pote palipoharibika. Nitazifanya mbuga zake kama shamba la Edeni, jangwa yake kama bustani ya Yawe. Ndani yake kutapatikana furaha na shangwe, na nyimbo za shukrani zitasikilika humo.


Kilio cha watu wa Hesiboni kinasikilika huko Eleale mpaka Yasa; kinaenea kutoka Soari mpaka Horonaimu na kufika hata Eglati-Selisia. Hata maji ya kijito Nimurimu yamekauka.


Dada yako mukubwa ni Samaria, aliyekaa upande wako wa kaskazini pamoja na wabinti zake. Dada yako mudogo ni Sodoma, aliyekaa upande wako wa kusini pamoja na wabinti zake.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu. Ulipambwa kwa kila namna ya mawe ya bei kali, akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili, sardoniki, yakuti samawi, almasi na zumaridi. Ulikuwa na mapambo ya zahabu. Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.


Kati ya miti ya mierezi ya bustani ya Mungu, hakuna muti uliolingana nao, wala misunobari haikulingana na matawi yake, mibambakofi haikuwa na matawi kama yake, hata muti wowote wa bustani ya Mungu haukulingana nao kwa uzuri.


Mimi niliufanya kuwa muzuri kwa matawi yake mengi; ulionewa wivu na miti yote ya Edeni iliyokuwa katika bustani ya Mungu.


Upande wa mashariki, mupaka utakuwa muto Yordani unaoelekea kati ya Haurani na Damasiki, Gileadi na inchi ya Israeli. Vilevile mupaka utapitia upande wa mashariki wa bahari ya Chumvi mpaka Tamari.


Kama vile moto unavyoteketeza, Jeshi hilo linaharibu kila kitu mbele yake na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa; mbele ya kupita kwao, inchi ni kama bustani ya Edeni, lakini wakisha kupita, ni jangwa tupu. Hakuna kinachoweza kuponyoka!


jangwa la Negebu na eneo la jangwa la bonde la Yeriko, muji wa miti ya ngazi mpaka Soari.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ