Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 12:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 12:8
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Akaendelea kusafiri toka eneo la Negebu mpaka Beteli. Alifika pahali alipokuwa amepiga kambi ya hema mara ya kwanza kati ya Beteli na Ai,


pahali ambapo alikuwa amejenga mazabahu. Pale Abramu akamwomba Yawe kwa jina lake.


Abrahamu akapanda muti wa mukwaju kule Beri-Seba, akaomba kwa jina la Yawe, akamwabudu Mungu, Mungu wa milele.


Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.


Kwa hiyo, Isaka akajenga mazabahu kule na kumwabudu Yawe. Akapiga kambi kule, na watumishi wake wakachimba kisima.


Akaita pahali hapo Beteli, ni kusema “Nyumba ya Mungu”. Jina la mbele la muji ule lilikuwa Luzi.


Basi, Labani akamufikia Yakobo. Wakati ule Yakobo alikuwa amepiga kambi yake kwenye milima. Labani naye, pamoja na wandugu zake, akapiga kambi yake kwenye milima ya Gileadi.


Basi, akajenga mazabahu pahali pale na kuiita “Mungu ni Mungu wa Israeli”.


Kisha, tutakwenda Beteli kusudi nimujengee Mungu mazabahu, Mungu ambaye alinisaidia siku ya taabu na kuwa nami popote nilipokwenda.”


Akajenga mazabahu pahali pale na kupaita “Mungu wa Beteli” maana ni pale ndipo pahali Mungu alipojionyesha kwake wakati alipokuwa akimukimbia kaka yake.


Seti naye akapata mutoto mwanaume, akamwita Enosi. Hapo ndipo watu walipoanza kumwomba Yawe kwa jina lake.


Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.


Watu wa kabila la Benjamina walikaa Geba, Mikimasi, Ai, Beteli na vijiji vinavyoizunguka.


Kisha nikamulilia Yawe: “Ee Yawe, tafazali uniokoe!”


Musa akajenga mazabahu na kuita mazabahu hiyo “Yawe ni Bendera Yangu”,


amefika katika muji wa Ayati. Amepitia kule Migoroni, mizigo yake ameiacha katika muji wa Mikimasi.


Halafu watu wote watakaoomba kwa jina la Bwana ataokolewa.’


Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


Walipofika kwenye muto Yordani wakiwa bado katika inchi ya Kanana, wakajenga mazabahu kubwa sana karibu na muto huo.


Yoshua akawatuma watu kutoka Yeriko kwenda muji wa Ai, unaokuwa karibu ya Beti-Aweni, upande wa mashariki wa Beteli, akawaambia: “Mwende muipeleleze inchi.” Nao wakaenda na kuupeleleza muji wa Ai.


Halafu akatwaa watu wengine elfu tano na kuwaweka wavizie kati ya muji wa Beteli na Ai, upande wa magaribi wa muji wa Ai.


Hakuna mutu yeyote aliyebaki katika muji wa Ai, waliuacha muji ule wazi wakaenda kuwafuatilia Waisraeli.


Basi, Yoshua akaondoka, pamoja na waaskari wake wote kwenda Ai. Akawachagua watu hodari elfu makumi tatu na kuwaambia watangulie wakati wa usiku.


Kisha, Yoshua akamujengea Yawe, Mungu wa Israeli, mazabahu juu ya mulima Ebali,


Basi, Yoshua akawaambia waende pahali pao pa kuvizia; nao wakajiweka upande wa magaribi wa muji wa Ai, kati ya muji wa Ai na Beteli. Lakini Yoshua akalala usiku huo katika kambi ya Waisraeli.


Gideoni akamujengea Yawe mazabahu kule na kuyaita, “Yawe ni Amani.” Mazabahu hiyo iko kule Ofura, muji wa Waabiezeri, mpaka leo.


Zawadi hizo zilikuwa kwa ajili ya wakaaji wa Beteli, wakaaji wa Ramoti katika Negebu, wakaaji wa Yatiri,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ