Mwanzo 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Abramu akapita katikati ya inchi mpaka Sekemu, pahali patakatifu, penye muti wa mwelo wa More. Wakati ule, Wakanana walikuwa ndio wenyeji wa inchi hiyo.
Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”
Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.
Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.
(Milima hii iko ngambo ya muto Yordani, upande wa magaribi wa barabara kuelekea upande jua linakotokea, katika inchi ya Wakanana wanaoishi Araba kuelekea Gilgali.)
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.
Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.
Mifupa ya Yosefu ambayo Waisraeli walikuwa wameileta kutoka Misri waliizika kule Sekemu katika eneo ambalo Yakobo alikuwa amelinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba ya Sekemu, kwa bei ya vikoroti mia moja vya feza. Eneo lile nalo likakuwa mali yao wazao wa Yosefu.
Yerubali, ni kusema Gideoni na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamuka mapema, wakapiga kambi yao katika bonde karibu na chemichemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wao wa kaskazini katika bonde karibu na mulima More.