Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 12:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Naye akamutendea Abramu mema kwa ajili ya Sarai. Akamupa kondoo, ngombe, punda dume, watumishi na wajakazi, punda dike na ngamia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 12:16
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na makundi ya nyama, feza na zahabu.


Hesabu ya nyama wao ilikuwa kubwa sana hata inchi ile haikuweza kutosha kwa Abramu na Loti kuishi pamoja.


Basi, Sarai, muke wa Abramu, alikuwa bado hajamuzalia mutoto, naye alikuwa na mujakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri.


Abimeleki akamurudishia Abrahamu muke wake Sara, akamupa kondoo, ngombe na watumwa na wajakazi.


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Alikuwa na makundi ya kondoo, ngombe na watumwa wengi. Kwa hiyo, Wafilistini wakamwonea wivu.


Basi, Yakobo akatajirika sana, akakuwa na makundi makubwa ya nyama, wajakazi na watumwa, ngamia na punda.


Akawapa maagizo haya: “Mutamwambia bwana wangu Esau hivi: Mutumishi wako Yakobo anasema hivi: ‘Nimekaa mugeni kwa Labani mpaka sasa.


Alikuwa na mali, kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, ngombe elfu moja, punda dike mia tano, na watumishi wengi sana. Yeye alikuwa wa heshima kuliko watu wote kule upande wa mashariki.


Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.


Lakini kama mutumishi yule akijisemesha mwenyewe kwamba bwana wake anakawia kurudia; na halafu anaanza kuwapiga watumishi wenzake, wanaume na wanawake, naye anakula na kunywa na kulewa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ