Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 12:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Wakubwa wa mufalme wa Misri walipomwona Sarai, wakamusifia kwa mufalme. Basi, Sarai akapelekwa ndani ya nyumba ya yule mufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 12:15
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Abramu alipofika Misri, wenyeji wa kule wakaona kwamba Sarai ni mwanamuke muzuri sana.


Akiwa kule, Abrahamu alisema kwamba muke wake Sara ni dada yake. Kwa hiyo, mufalme Abimeleki wa Gerari akamutwaa Sara.


Watu wa kule walipomwuliza juu ya muke wake, akajibu: “Huyu ni dada yangu.” Aliogopa kusema kwamba ni muke wake kwa kuogopa kwamba wakaaji wa inchi wangemwua kwa sababu ya Rebeka, maana Rebeka alikuwa muzuri sana.


Mufalme wa Misri akawakasirikia wale wakubwa wake wawili,


Ilipofika mwisho wa miaka miwili mizima, mufalme wa Misri akaota ndoto: alijikuta amesimama kando ya muto Nili,


Solomono alifanya mapatano na mufalme wa Misri, kwa kumwoa binti yake. Akamuleta binti wa mufalme wa Misri na kumuweka katika muji wa Daudi, mpaka alipomaliza kujenga nyumba yake mwenyewe, nyumba ya Yawe, na ukuta wa kuuzunguka Yerusalema.


Angalia sasa. Unategemea Misri, utete uliovunjika ambao utamuchoma mukono mutu yeyote atakayeutegemea. Hivi ndivyo mufalme wa Misri anavyokuwa kwa wote wale wanaomutegemea.


Mumutafute Yawe mwenye nguvu; mumutafute Yawe siku zote.


Naye mufalme wa Misri aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumwua Musa. Lakini Musa akamukimbia mufalme, akaenda kukaa katika inchi ya Midiani. Siku moja, Musa alikuwa akikaa kando ya kisima cha maji.


Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae.


Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.


Ndivyo mwanaume anayelala na muke wa mwenzake anavyokuwa; yeyote anayemugusa mwanamuke yule hataacha kuazibiwa.


Mufalme wa Misri, wasimamizi wake na wakubwa wa serikali yake pamoja na watu wake wote;


Naye Mufalme wa Misri, mumupange jina hili: Mwenye domo ya bure!


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ