Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”
Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”
Na kwa ngambo yenu ninyi watu wa Israeli, ninaleta taifa moja kutoka mbali kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hili taifa haliwezi kushindwa, ni taifa la zamani, ni taifa ambalo hamufahamu luga yake. Hamuwezi kuelewa hata neno wanalolisema.
Basi kama kanisa zima limekusanyika, na watu wote wanaanza kusema kwa luga za ajabu; na kisha watu wasioelewa kitu au wasioamini wakiingia katika mukutano wenu hawatasema kuwa ninyi ni wenda-wazimu?