Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 11:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Yawe akasema: “Watu hawa ni taifa moja na wote wana luga moja; huu ni mwanzo tu wa yale watakayofanya. Jambo lolote wanalokusudia kufanya watafanikiwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 11:6
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wote katika dunia walikuwa na luga moja, walitumia maneno mamoja.


Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”


Yawe alipoona uwingi wa uovu wa watu katika dunia, na kwamba kila kitu mwanadamu anachokusudia ndani ya moyo wake ni kiovu siku zote,


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Hao ndio wana watatu wa Noa na kutokana nao watu walienea katika dunia yote.


Ilipofika saa sita muchana, Elia akaanza kuwachekelea akisema: “Muombe kwa sauti kubwa zaidi! Yeye ni mungu, labda iko na kazi nyingi au ametoka na kusafiri! Labda analala, munapaswa kumwamusha!”


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Tena niliwanyima mvua miezi mitatu tu mbele ya mavuno. Nilinyeshea mvua muji mumoja, na muji mwingine nikaunyima. Shamba moja lilipata mvua, na lingine halikupata, likakauka.


Ametenda kwa uwezo wake mukubwa, amewasambaza wale wanaofanya mipango kwa kiburi.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


Muende muililie hiyo miungu muliyoichagua. Muache hiyo iwakomboe katika taabu zenu!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ