Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 11:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Wakasema: “Tujijengee muji na munara ambao chongo yake itafika mbinguni kusudi tujipatie sifa, kusudi tusisambazwe katika dunia yote.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 11:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika siku zile na hata kisha, kulikuwa majitu katika dunia ambao walikuwa wazao wa wana wa Mungu na wabinti za wanadamu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa wa zamani, na waliitwa Wanefili.


Daudi alijiongezea sifa yake. Alipokuwa anarudi kisha kumushinda Hadadezeri, aliwaua Waedomu elfu kumi na nane, katika Bonde la Chumvi.


Walitupwa juu angani, kisha chini ndani ya shimo; uhodari wao ukawaishia katika tukio lile.


Lakini wewe, ee Yawe, ni mukubwa kwa milele.


Mwenye haki anakumbukwa kwa baraka, lakini waovu watasahauliwa kabisa.


Ingawa Babeli ungepanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha kuta zake ndefu, waangamizaji watakuja kutoka kwangu kwa kuuharibu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Akalalamika kwa sauti akisema: Mukate muti huu na kuyakatakata matawi yake. Muangushe majani yake na kuyatawanya matunda yake. Nyama wakimbie toka chini yake na ndege kutoka matawi yake.


Wewe utafukuzwa mbali na wanadamu. Utaishi pamoja na nyama wa pori, utakula majani kama ngombe; utalowana na umande wa mbinguni. Utakaa katika hali hiyo kwa miaka saba, na kwa mwisho utatambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya ufalme wa wanadamu naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Ametenda kwa uwezo wake mukubwa, amewasambaza wale wanaofanya mipango kwa kiburi.


Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


Kwa nini tuende huko wakati tumevunjika moyo kwa hofu? Wametuambia kwamba watu wa huko ni wakubwa na warefu kuliko sisi, na kwamba miji yao ni mikubwa na yenye kuta zinazofika katika mawingu. Tena wamesema kwamba waliwaona wale wazao wa Anaki!’


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


“Musikilize enyi Waisraeli! Hivi leo mumekaribia kuvuka muto Yordani, kwenda kurizi inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi. Miji yao ni mikubwa na ina kuta zinazofika katika mawingu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ