Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.
Halafu aliwakamata watu wa muji ule, akawaweka kwa kazi ya kutumikisha misumeno, sururu za chuma, mashoka ya chuma na kuwatumia kufanya kazi katika furu ya matofali. Hivi ndivyo alivyoitendea miji yote ya Waamoni. Kisha Daudi na watu wote walirudi Yerusalema.
Wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shamba. Katika kazi zile zote, Waisraeli walitumikishwa kwa kinguvu.
Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo, akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani.
Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.
Lakini muonyane kila siku kwa muda wote ambao lile neno “leo” linalotajwa lingali linatuelekea kusudi hata mumoja wenu asikuwe mugumu kwa kudanganywa na zambi.
Munisikilize sasa, ninyi munaosema: “Leo au kesho tutakwenda katika muji fulani, tutakaa kule kwa muda wa mwaka muzima, tutafanya biashara na kupata faida.”