Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.
Kwa hiyo, Abramu akaondoka kama vile Yawe alivyomwamuru, na Loti akakwenda pamoja naye. Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi saba na mitano alipotoka Harani.
Alitwaa Sarai muke wake, na Loti mwana wa ndugu yake, pamoja na mali yao yote na watu wote waliokuwa wamejipatia kule Harani, wakaondoka kuelekea inchi ya Kanana. Walipoingia katika inchi ya Kanana,
Yoshua akawaambia watu wote: “Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Hapo zamani, wazee wenu waliishi ngambo ya muto Furati, wakaitumikia miungu mingine. Muzee mumoja aliitwa Tera, baba ya Abrahamu na Nahori.