Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kutokana na hawa visanga vya watu wa mataifa mengine vikagawanywa kwa inchi zao, kila watu kwa luga yao, kwa jamaa zao, kufuatana na mataifa yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 10:5
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hao ndio wazao wa Hamu kufuatana na makabila yao, luga zao, inchi zao na mataifa yao.


Eberi alikuwa na wana wawili: wa kwanza akamwita Pelegi kwa sababu wakati ule watu katika dunia waligawanyika na wa pili akamwita Yokitani.


Hao ndio jamaa za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao na mataifa yao. Kutokana nao, mataifa yote yalienea katika dunia nyuma ya mafuriko ya maji.


Wana wa Yavani walikuwa Elisa, Tarsisi, Kitimu na Rodanimu.


Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misiraimu, Puti na Kanana.


Hao ndio wana watatu wa Noa na kutokana nao watu walienea katika dunia yote.


Mufalme Ahasuero alilipisha kodi kwa watu wa inchi na katika visanga vya bahari.


Wafalme wa Tarsisi na visiwa wamulipe kodi, wafalme wa Sheba na Seba wamuletee zawadi.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


na wale wa upande wa mashariki wanamusifu. Watu wa mbali wanalisifu jina la Yawe, Mungu wa Israeli.


Kwake mataifa ni kama tone la maji katika mbeketi, ni kama mavumbi juu ya kilo. Kwake visanga ni vyepesi kama mavumbi laini.


Wakaaji wa mbali wameona mambo niliyotenda, wakaogopa; dunia yote inatetemeka kwa woga. Watu wote wamekusanyika, wakakuja.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.


Munisikilize, enyi inchi za mbali, Mutege sikio, enyi watu wa mbali! Yawe aliniita mbele sijazaliwa, alitaja jina langu nikiwa katika tumbo la mama yangu.


Ukombozi wangu unakaribia upesi; wokovu nitakaoleta unaanza kutokea. Mimi mwenyewe nitayatawala mataifa. Wakaaji wa inchi za mbali wananingojea, wanaitegemea nguvu yangu.


Atawaazibu waadui kadiri ya matendo yao, kasirani yake na kisasi vitawapata waadui zake; atawaazibu hata wakaaji wa inchi za mbali.


Ni mashua zinazotoka katika inchi za mbali, zikitanguliwa na mashua za Tarsisi. Zinawaleta watoto wako, pamoja na feza na zahabu yao, kwa sifa ya Yawe, Mungu wako, kwa sifa ya Mungu, Mutukufu wa Israeli, maana amewafanya mupate utukufu.


Basi muvuke bahari mpaka Kipuro, muone, au mutume watu huko Kedari wachunguze, kama jambo kama hili limekwisha kutokea.


wafalme wote wa Tiro na Sidona; wafalme wa inchi zinazokuwa kandokando ya bahari ya Mediteranea;


Bwana wetu Yawe anasema hivi kwa Tiro: Wakaaji wa sehemu za kandokando ya bahari watatetemeka watakaposikia kishindo cha kuanguka kwako na mulio wa maumivu na wa watu wanaouawa.


Sasa watu wa visanga wanatetemeka kwa sababu ya kuanguka kwako; watu wa visanga katika bahari wanatishwa kwa kuanguka kwako!


Nyuma ya hayo, atageukia na kushambulia inchi nyingi za kandokando ya bahari na kuzishinda. Lakini jemadari mugeni atamushinda na kuyakomesha majivuno yake mwenyewe; kweli atamurudishia mufalme wa kaskazini majivuno yake mwenyewe.


Wao watamwogopa sana Yawe; ataiangamiza miungu yote ya dunia. Mataifa yote katika dunia yatamwabudu; kila taifa katika pahali pake.


Mungu Mukubwa alipogawanyia mataifa mali yao, alipowagawanyia wanadamu, kila taifa alilipatia mipaka yake, kulingana na hesabu ya wamalaika,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ