31 Hao ndio wazao wa Semu, kufuatana na makabila yao, luga zao, inchi zao na mataifa yao.
Hao ndio wazao wa Hamu kufuatana na makabila yao, luga zao, inchi zao na mataifa yao.
Inchi walimokaa ilienea toka Mesa mpaka Sefari katika inchi ya vilima vya upande wa mashariki.
Hao ndio jamaa za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao na mataifa yao. Kutokana nao, mataifa yote yalienea katika dunia nyuma ya mafuriko ya maji.
Kutokana na hawa visanga vya watu wa mataifa mengine vikagawanywa kwa inchi zao, kila watu kwa luga yao, kwa jamaa zao, kufuatana na mataifa yao.
Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.