Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mungu akasema: “Maji yanayokuwa chini ya mbingu yakusanyike pahali pamoja, inchi kavu itokee.” Ikakuwa hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 1:9
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akaliita anga “Mbingu”. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya pili.


Ezra akaomba akisema: Wewe peke yako ndiwe Yawe! Ulifanya mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake. Unavipatia uzima, na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.


Amechora muviringo juu ya uso wa bahari, penye mpaka kati ya mwangaza na giza.


Mungu anatandaza kaskazini juu ya pahali patupu, na anatundika dunia pahali pasipo kuwa kitu.


umejenga makao yako katika mbingu juu ya maji. Umeyafanya mawingu kuwa gari lako nawe unatembea katika anga.


Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.


Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya; kwa mikono yake aliumba inchi kavu.


Mito yote inatiririkia ndani ya bahari, lakini bahari haijai hata kidogo; kule ambako mito inatiririkia ndiko kule inaendelea kwenda.


Mbona hamuniogopi? –Ni ujumbe wa Yawe.– Kwa nini hamutetemeki mbele yangu? Mimi niliwekea bahari muchanga kuwa mupaka wake; ni kizuizo cha milele ambacho bahari haiwezi kuvuka. Ingawa mawimbi yanaupiga, hayawezi kuupita; ingawa yanavuma, hayawezi kuuruka.


Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.


Watu hawa wanasahau kwa makusudi kwamba tangia zamani Mungu alisema tu, na mbingu na dunia vikakuwa. Dunia iliumbwa toka katika maji na kwa njia ya maji.


Akaapa kwa jina la Mungu anayeishi kwa milele na milele, muumba wa mbingu na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, nayo dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, pamoja na bahari na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake, na kusema: “Hakutakuwa tena muda unaobaki!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ