Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Mungu akasema: “Mwangaza ukuwe.” Mwangaza ukakuwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 1:3
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa. Siku ile Yawe Mungu alipoumba mbingu na dunia,


Yeye anatandaza umeme wake kumuzunguka, na kuvifunika vilindi vya bahari.


Makao ya mwangaza yako wapi? Kwenye nyumba ya giza ni wapi,


Umejifunika mwangaza kama kanzu, umekunjua mbingu kama hema;


Yawe ni Mungu; yeye ametujalia mwangaza wake. Mushike matawi katika mikono, mukiandamana mpaka kwenye mazabahu.


Vyote visifu jina la Yawe, maana yeye aliamuru, na vyote vikakuwa.


Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Mwangaza unamwangazia mutu wa haki, nayo furaha ni kwa watu wenye moyo wa usawa.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Hautahitaji tena jua kukuangazia muchana, wala mwezi kukuangazia usiku; maana mimi Yawe ni mwangaza wako milele; mimi Mungu wako nitakuwa utukufu wako.


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.


Mwangaza ule uliangaza katika giza, wala giza halikuuzimisha.


Ule mwangaza wa kweli, unaomwangazia kila mutu, unakuja katika dunia.


Wakati alipokwisha kusema maneno haya, akaita kwa sauti kubwa, akisema: “Lazaro, toka inje.”


Hukumu inatokana na hivi: mwangaza umekuja katika ulimwengu, lakini watu wanapenda giza kuliko mwangaza, kwa sababu matendo yao ni mabaya.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi: “Amuka wewe unayelala! Ufufuke kutoka kati ya wafu, naye Kristo atakuangazia.”


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kutoka kwa Yesu Kristo na kuitangaza kwenu: Mungu ni mwangaza, na ndani yake hamuna giza hata kidogo.


Kwa ngambo ingine amri hii ninayowaandikia ni mupya, na ukweli wake unaonekana ndani ya Kristo na ndani yenu vilevile. Kwa maana giza linapita na mwangaza wa kweli umekwisha kutokea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ