Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 1:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Mungu akasema: “Inchi itoe aina zote za viumbe vyenye uzima: nyama wa kufugwa, viumbe vinavyotambaa na nyama wa pori wa kila aina.” Ikakuwa hivyo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 1:24
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tano.


Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.


“Utaingiza kila aina ya ndege wa anga, kila aina ya nyama, kila aina ya kiumbe kinachotambaa, wawili wa kila aina, kwa kuwalinda wazima.


Waliingia wao wenyewe pamoja na aina zote za nyama wa pori, aina zote za nyama wanaofugwa, aina zote za nyama wanaotambaa na ndege wa kila aina.


Wakatoka, kufuatana na jamii zao, nyama wote wa pori, viumbe vyote vinavyotambaa, ndege wote na nyama wote wenye uzima katika dunia.


Unajua mbuzi wa milima anazaa wakati gani, au umekwisha kuona kulungu akizaa?


Yobu, ni wewe ndiwe uliyewapa farasi nguvu, ukawavalisha kwenye shingo manyoya marefu?


Nani aliyemwacha huru punda wa pori? Nani aliyewaacha waende kwa kuwafungua?


Mbogo atakubali kukutumikia? Atakubali kulala katika zizi lako?


Uangalie yule nyama mukubwa kiboko. Nilimwumba kama nilivyokuumba wewe. Yeye anakula majani kama ngombe,


Milima mirefu ni makao ya mbuzi wa pori; makimbilio ya sungura wa pori ni chini ya mawe.


Hapo mwanadamu naye anaenda kwenye kazi zake; naye anatumika mpaka magaribi.


Mumusifu, enyi nyama wa pori na wa kufugwa, viumbe vinavyotambaa na ndege wote!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ