Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mungu akaumba nyama wakubwa sana wa bahari na aina zote za viumbe vyenye uzima vinavyotembea ndani ya maji. Akaumba aina zote za ndege. Mungu akaona kwamba ni vizuri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 1:21
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

ipate kutawala muchana na usiku, na kutenga mwangaza na giza. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


Mungu akasema: “Maji yajae makundi ya viumbe vyenye uzima. Na ndege waruke katika anga.”


Mungu akavibariki, akasema: “Muzae, muongezeke, mujaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika inchi.”


Mungu akafanya aina zote za nyama wa pori, nyama wa kufugwa, na viumbe vinavyotambaa. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


Mungu akaona kwamba kila kitu alichofanya ni kizuri kabisa. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya sita.


Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.


“Utaingiza kila aina ya ndege wa anga, kila aina ya nyama, kila aina ya kiumbe kinachotambaa, wawili wa kila aina, kwa kuwalinda wazima.


Waliingia wao wenyewe pamoja na aina zote za nyama wa pori, aina zote za nyama wanaofugwa, aina zote za nyama wanaotambaa na ndege wa kila aina.


Ondoa vilevile viumbe vyote vyenye uzima vya kila aina vilivyokuwa pamoja nawe, ndege na nyama na kila kiumbe kinachotambaa, vipate kuzaa kwa wingi katika dunia, viongezeke na kuenea kila pahali katika dunia.”


Wakatoka, kufuatana na jamii zao, nyama wote wa pori, viumbe vyote vinavyotambaa, ndege wote na nyama wote wenye uzima katika dunia.


Nyama wote, ndege wote wa anga, viumbe vyote vinavyotambaa juu ya inchi na samaki wote wa bahari watakuwa na hofu na kuwaogopa ninyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu.


Nanyi muzae, mwongezeke, muzae kwa wingi, mwongezeke katika inchi.”


Lakini uulize nyama nao watakufundisha; uulize ndege nao watakuambia.


Mizimu kule chini inatetemeka, maji ya chini na wakaaji wake yanaogopa.


Mimi ni bahari au nyama mukubwa wa bahari hata upate kuniwekea mulinzi?


Mumusifu Yawe tokea katika dunia; enyi nyoka wakubwa wa bahari na mashimo ya bahari, mumusifu.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao vilevile wakaleta vyura katika inchi ya Misri.


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.


Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani, nitakutolea sadaka, na kutimiza viapo vyangu. Yawe, ndiye anayeokoa.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ