Mwanzo 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Mungu akaumba nyama wakubwa sana wa bahari na aina zote za viumbe vyenye uzima vinavyotembea ndani ya maji. Akaumba aina zote za ndege. Mungu akaona kwamba ni vizuri.
Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.
Ondoa vilevile viumbe vyote vyenye uzima vya kila aina vilivyokuwa pamoja nawe, ndege na nyama na kila kiumbe kinachotambaa, vipate kuzaa kwa wingi katika dunia, viongezeke na kuenea kila pahali katika dunia.”
Nyama wote, ndege wote wa anga, viumbe vyote vinavyotambaa juu ya inchi na samaki wote wa bahari watakuwa na hofu na kuwaogopa ninyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu.
Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa kuomboleza juu ya Mufalme wa Misri. Wewe Mufalme wa Misri unajiona kuwa simba kati ya mataifa, lakini wewe ni kama mamba tu katika maji: unachomoka kwa nguvu kwenye mito yako, unayavuruga maji kwa miguu yako, na kuichafua mito.
Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.