Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 7:2
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

anajificha katika maficho yake kama simba. Anavizia apate kuwakamata wamasikini; anawanasa kwa mutego wake na kuwachukua.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa vyombo vyenye nyuzi nane. Zaburi ya Daudi.


Unisaidie, ee Yawe! Watu wema wamekwisha; waaminifu wametoweka kati ya watu.


Utukuzwe, ee Mungu, juu katika mbingu! Utukufu wako uenee katika dunia yote!


Wakisema: “Twende kuvizia mutu na kumwua; kuja tuwashambulie wasiokuwa na kosa!


Maneno ya waovu shabaha yake ni kuua, lakini kinywa cha mutu wa usawa kinaokoa.


Watu watatesana, kila mutu na mwenzake; vijana watawazarau wazee, na watu wa ovyo ovyo watawazarau wenye heshima.


Mutu wa haki akikufa, hakuna mutu anayejali; mutu mwema akihamishwa toka dunia, hakuna mutu anayefikiri na kusema: Mutu huyo mwema amehamishwa kusudi asipatwe na hasara,


Muko mbio kutenda maovu, muko wepesi kumwanga damu isiyokuwa na kosa. Mawazo yenu ni mawazo ya uovu, popote munapokwenda munaacha ukiwa na uharibifu.


wananyanganya upande mumoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mumoja anamushambulia mwenzake.


Nitaita wavuvi wengi kuja kuwanasa watu hawa. Kisha, nitaita wawindaji wengi kuja kuwawinda juu ya kila mulima, kila kilima na katika mapango ya chini ya mawe.


Mishale yao inaua watu kwa uwingi, wote ni mashujaa wa vita.


Hakika, kati ya watu wangu kuna waovu, watu ambao wananyanganya mali za wengine. Wako kama wawindaji wa ndege: wanatega mitego yao na kuwanasa watu.


Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.


Watu walifuatilia hatua zetu, tukashindwa kupita katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikaribia, siku zetu zilitimia, mwisho wetu ulifika.


Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ole kwake muji wa mauaji! Muji huo ni kama chungu chenye kutu, ambacho kutu yake haiwezi kutoka! Vipande vya nyama ndani yake vinatoshwa kimoja kimoja bila kuchaguliwa.


Musikilize, enyi makuhani! Mutege sikio, enyi Waisraeli! Musikilize, enyi ukoo wa kifalme! Ninyi mulipaswa kulinda haki, pahali pake mumekuwa kama mutego kule Misipa, mumekuwa kama wavu wa kuwanasa kule Tabori.


Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.


Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi: Munawatendea watu wangu kama adui. Munawanyanganya watu watulivu nguo zao; watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi, na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.


Ninyi munajenga Sayuni kwa damu, Yerusalema kwa uovu.


Lakini ninyi munachukia mazuri na kupenda mabaya. Munawachuna ngozi watu wangu, na kunyofoa nyama juu ya mifupa yao.


Sitawahurumia tena wakaaji wa dunia. Nitamwacha kila mutu katika mikono ya mwenzake, na kila mwanainchi katika mikono ya mufalme wake. Nao wataiangamiza dunia, nami sitamwokoa mutu yeyote toka katika mikono yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wayuda wakamwunga mukono, wakisema kwamba maneno yale yote ni ya kweli.


Sasa, leo umejionea kwa macho yako mwenyewe. Ulipokuwa ndani ya pango Yawe alikutia katika mikono yangu. Wamoja kati ya watu wangu waliniambia nikuue, lakini nilikuhurumia. Nikasema sitanyoosha mukono wangu juu ya bwana wangu maana yeye ni muchaguliwa wa Yawe.


Usiniache nikufe katika inchi ya kigeni, mbali na Yawe. Kwa nini wewe mufalme wa Israeli umetoka kuyatafuta maisha yangu kama mutu anayewinda kwale juu ya milima?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ