Mika 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Siku hiyo wandugu zenu watawarudilia, kutoka Asuria na vijiji vya Misri, kutoka inchi ya Misri na eneo la muto Furati; kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.
Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.
Nitawarudisha kutoka inchi ya kaskazini, nitawakusanya kutoka miisho ya dunia. Wote watakuwa pale; hata vipofu na vilema, wanawake wenye mimba na wanaosikia maumivu ya kuzaa; kundi kubwa sana la watu litarudi hapa.
Lakini wewe usiogope, ee Yakobo mutumishi wangu, usifazaike, ee Israeli, maana nitakuokoa kutoka mbali, nitakuja kuwaokoa wazao wako kutoka inchi walimohamishiwa. Yakobo utarudi na kutulia na kustarehe, wala hakuna yeyote atakayekutia hofu.
uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitawatoa Waisraeli kutoka mataifa walikokwenda; nitawakusanya toka pande zote na kuwarudisha katika inchi yao.