Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 7:10
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Niliwatwanga, wakakuwa kama mavumbi, nikawaponda na kuwakanyaga kama matope katika barabara.


Waadui zangu wazungukwe na mazarau; wajifunike haya yao kama vile nguo.


Kwa nini mataifa yanasema: “Mungu wenu yuko wapi?”


Walitafuta musaada, lakini hakukukuwa wa kuwasaidia; walimulilia Yawe, lakini hakuwajibu.


Uwaache hao wanaofurahia hasara yangu, washindwe wote na kufezeheka. Hao wote wanaojiona bora kuliko mimi, wapate haya na kufezeheka.


Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”


Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?


Mbele hawajatambua, waongolewe kama miiba, michongoma au magugu. Kwa hasira ya Mungu, wapeperushwe mbali, wakikuwa bado wazima.


Kwa nini mataifa yatuambie: “Mungu wenu yuko wapi?” Utujalie tuone jinsi utakavyowalipiza mataifa kisasi kwa ajili ya mauaji ya watumishi wako.


Kwa macho yangu, nimeona waadui zangu wameshindwa; kwa masikio yangu, nimesikia kilio cha wanaotenda maovu.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Mimi Yawe nitakufanya wewe Edomu kuwa mudogo kuliko mataifa yote. Ulimwengu wote utakuzarau.


Nitaiazibu Babeli na wakaaji wote wa Kaldea mukiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Watavaa gunia, hofu itawashika, nao watapata haya na vichwa vyao vyote vitanyolewa.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?


Kwa sababu ya mateso makali muliyowatendea wandugu zenu wazao wa Yakobo, mutafezeheshwa na kuangamizwa milele.


Hamukupaswa kuangalia tu siku hiyo wandugu zenu walipopatwa na taabu, hamukupaswa kufurahi juu ya Wayuda siku hiyo walipoangamizwa, hamukupaswa kujivuna siku ile wenzenu walipokuwa wanateseka,


Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia. Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe, nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!


Usifurahie hali yangu ewe adui yangu! Nikianguka, nitasimama tena; nikiwa katika giza, Yawe ni mwangaza wangu.


Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Nanyi mutakapoyaona mambo yale kwa macho yenu, mutatambua na kusema: Ukubwa wa Yawe unafika hata inje ya mipaka ya inchi ya Israeli.


Yeye alimutumainia Mungu na alisema kwamba yeye ni Mwana wa Mungu. Ikiwa Mungu anapendezwa naye sasa amwokoe!”


Basi, Wakanana pamoja na wakaaji wote wa inchi hii watakapopata habari hiyo watatuzunguka na kutufuta kabisa katika dunia. Sasa utafanya nini kwa kuonyesha ukubwa wa jina lako?”


Enyi mbingu, nanyi watu wa Mungu pamoja na mitume na manabii wake, mufurahi kwa ajili ya mambo yaliyotokea muji ule, kwa maana Mungu amewapatia haki yenu kwa kuuhukumu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ