Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 6:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alipovikaripia, pumzi ya pua yake ilifunua vilindi vya bahari na misingi ya dunia ikaonekana.


Halafu, dunia ikatetemeka na kutikisika, misingi ya mbinguni ikayumbayumba na kuruka, kwa maana Mungu alikuwa amekasirika.


Umeiweka dunia imara juu ya misingi yake, isitikisike hata milele.


wakati alipowekea bahari mupaka wake kusudi maji yake yasipate kuvunja amri yake, wakati alipoweka misingi ya dunia.


Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.


Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake.


Munikumbushe tena makosa yangu, tusambe nanyi, mutoe mashitaki yenu kusudi tuuone ukweli wenu!


Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi: Enyi wakaaji wa Yerusalema na watu wa Yuda, tafazali mukuwe waamuzi kati yangu na shamba langu.


Kwa hiyo, mimi nitawashitaki ninyi, na nitawashitaki wazao wenu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Vishindo hivyo vitasikilika mpaka mwisho wa dunia, maana Yawe ana mashitaki juu ya mataifa; anawahukumu wanadamu wote, naye atawaua waovu kwa upanga! –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Kama mbingu zinaweza kupimwa, na misingi ya dunia kuchunguzwa, basi, nitawatupilia wazao wa Israeli, kwa sababu ya mambo yote waliyotenda.


Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Musikilize jinsi Yawe anavyosema: Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima, navyo vilima visikie sauti yako.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ