Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 6:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 6:16
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Na nyumba hii itaharibiwa na kuwa mabomoko. Kila mutu atakayepita karibu atashituka na kutikisa kichwa, na kuuliza: ‘Kwa nini Yawe amefanya hivyo kwa inchi hii na kwa nyumba hii?’


lakini alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli. Akamutambikia hata mwana wake kwa kuteketezwa kwa moto, akifuata desturi mbaya za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe wakati Waisraeli walipokuwa wanaingia katika inchi.


Alitengeneza upya nafasi za kuabudia miungu mingine zilizoharibiwa na baba yake Hezekia. Akajenga mazabahu za kuabudia Bali na kutengeneza sanamu ya Ashera, kama vile Ahabu mufalme wa Israeli alivyofanya. Vilevile, Manase aliabudu na kutumikia jeshi la mbingu.


Alitenda maovu mbele ya Yawe kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya maana hao ndio waliokuwa washauri wake nyuma ya kifo cha baba yake, mpaka kwa kuangamia kwake.


Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.


Heri mutu asiyefuata shauri la waovu, asiyeshiriki katika njia ya wenye zambi, wala kukusanyika na wenye kuzarau;


Umeuzisha watu wako kwa bei ya chini; wala haukupata faida yoyote.


Umetupotezea heshima mbele ya jirani zetu, nao wanatuchekelea na kutuzarau.


Bwana wetu Yawe atakiangamiza kifo milele! Atayafuta machozi katika nyuso za watu wote na kuondoa haya ya watu wake katika dunia yote. Yawe amesema hivyo.


Kwa hiyo, Yawe hawahurumii vijana wao, hana huruma juu ya wayatima na wajane wao; maana hakuna hata mumoja anayemufuata, kila mutu anasema upumbafu. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Nitaufanya muji huu kuwa pahali pa kushangaza; nitaufanya kuwa kitu cha kuzomewa. Kila mutu anayepita karibu nao atashangaa na kuuzomea kwa sababu ya hasara zote zitakazowapata.


Kwanza nikakunywesha wakaaji wa Yerusalema na miji mingine ya Yuda, wafalme wake na wakubwa wa serikali yake kusudi ikuwe jangwa, ukiwa, kitu cha kuzomewa na cha kulaaniwa, kama inavyokuwa mpaka leo. Halafu nikakunywesha:


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.


Ninyi munasema: Tumepatishwa haya na kutukaniwa; haya imefunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Yawe.


Lakini wao hawakunitii wala kunitegea sikio. Lakini wakafuata mashauri yao wenyewe na ugumu wa mioyo yao, wakarudi nyuma pahali pa kusonga mbele.


Ukumbuke, ee Yawe, mambo yaliyotupata! Utuangalie, uone haya yetu!


Watakapokuwa wanaishi kwa usalama katika inchi yao, bila kutishwa, watasahau haya yao na uasi walionitendea.


Ee Bwana, kwa kadiri ya matendo yako ya haki usiukasirikie wala kuwa na hasira kwa ajili ya muji wako Yerusalema, mulima wako mutakatifu. Watu wote wa inchi za jirani wanauzarau Yerusalema na watu wako, kwa sababu ya zambi zetu na maovu babu zetu waliyotenda.


Kwa njia ya nabii, Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri. Kwa njia ya nabii, Mungu aliwalinda.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Usituhubirie sisi. Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa. Sisi hatutapatwa na hasara!


Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini, na kuwaangamiza kwa sababu ya zambi zenu.


Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ