Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Musikilize jinsi Yawe anavyosema: Wewe nabii, kwenda ukailalamikie milima, navyo vilima visikie sauti yako.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 6:1
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaburi ya Asafu. Mungu, Mungu Yawe, amesema, amewaita wakaaji wa dunia, tokea magaribi mpaka mashariki.


Kutoka juu anaita mbingu na dunia kuwa washuhuda wake atakapowahukumu watu wake.


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake.


Enyi Waisraeli, musikilize kwa uangalifu, musikuwe na kiburi maana Yawe anasema nanyi.


Ee inchi, ee inchi, ee inchi! Sikia neno la Yawe!


Yawe aliniambia hivi: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya milima ya Israeli. Uiambie isikilize maneno yangu.


Lakini juu ya milima ya Waisraeli, miti itatoa matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Waisraeli, maana wao wanakaribia kurudi katika inchi yao.


Naye akaniambia: Toa unabii juu ya mifupa hii. Uiambie hivi: Enyi mifupa yenye kukauka, musikilize neno la Yawe.


na kusema hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe, enyi wakaaji wa milima ya Israeli! Anawaambia ninyi wakaaji wenye kuwa katika milima na vilima na katika maporomoko na mabonde kwamba: Mimi mwenyewe, Bwana wenu Yawe, nitaleta upanga na kuharibu sehemu zenu zote zilizoinuka za kutambikia.


Enyi Waisraeli, musikilize neno Yawe alilosema juu yenu, enyi taifa zima alilolitoa katika inchi ya Misri:


Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.


Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.


Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.


Yesu akawajibu: “Ninawaambia ninyi: kama watu hawa wakinyamaza, mawe yatalalamika.”


Utege sikio, ee mbingu. Sikiliza, ee dunia, maneno ninayosema.


Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.


Samweli akamwambia Saulo: “Nyamaza! Nitakuambia jambo Yawe aliloniambia leo usiku.” Saulo akasema: “Uniambie.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ