Lakini juu ya milima ya Waisraeli, miti itatoa matawi na kuzaa matunda kwa ajili ya watu wangu Waisraeli, maana wao wanakaribia kurudi katika inchi yao.
na kusema hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe, enyi wakaaji wa milima ya Israeli! Anawaambia ninyi wakaaji wenye kuwa katika milima na vilima na katika maporomoko na mabonde kwamba: Mimi mwenyewe, Bwana wenu Yawe, nitaleta upanga na kuharibu sehemu zenu zote zilizoinuka za kutambikia.
Musikilize enyi watu wote; sikiliza ewe dunia na vyote vinavyokuwa ndani yako. Bwana wetu Yawe anakuja kuwashitaki, Bwana wetu anasema kutoka hekalu lake takatifu.
Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.
Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.