Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 5:2
57 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo na jamaa yake yote wakaendelea na safari yao kutoka Beteli. Walipokuwa umbali fulani mbele ya kufika Efurata, Rakeli akashikwa na uchungu mukali wa kuzaa.


Basi, Rakeli akakufa na kuzikwa kando ya njia inayokwenda Efurata, ni kusema Betelehemu.


Ninaamua hivyo kwa sababu ya mama yako, Rakeli. Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani yeye alikufa katika inchi ya Kanana, tukiwa karibu kufika Efurata, akaniachia huzuni. Basi, nikamuzika palepale, kando ya njia inayokwenda Efurata, maana yake Betelehemu.”


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Salma, mwanzilishi wa muji wa Betelehemu alikuwa babu ya: Wanetofati, Waataroti-Beti-Yoabu na nusu ya Wamenahati ni kusema Wazori.


Penueli alizaa Gedori na Ezeri, na Ezeri alizaa Husa. Hawa ndio wazao wa Huri muzaliwa wa kwanza wa Efurata, watu wa muji wa Betelehemu.


Ingawa kabila la Yuda ndilo lililokuja kuwa lenye nguvu zaidi kuliko mengine, na watawala walitoka mule, haki ya muzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu).


Tulisikia wakisema: “Sanduku la Agano ni kule Efurata, tulilikuta katika mashamba ya Yearimu.”


Mbele milima haijakuwa, mbele haujauumba ulimwengu, wewe ndiwe Mungu, milele na milele.


Lakini juu ya mambo mengine, chagua kati ya watu wote, watu wanaostahili, watu wanaomwogopa Mungu, waaminifu na wanaochukia kituliro. Uwape hao mamlaka, wakuwe na kazi ya kuwasimamia watu katika makundi ya watu elfu, mia, makumi tano na kumikumi.


Basi, akachagua watu wenye uwezo kati ya Waisraeli, akawafanya kuwa viongozi wa makundi ya watu elfu, watu mia, watu makumi tano na watu kumikumi.


Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.


Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Mwongozi wao atakuwa mumoja wao, mutawala wao atatokea katikati yao. Nitamuruhusu kuwa karibu nami; maana, ni nani anayeweza kusubutu kuhatarisha uzima wake kwa kunikaribia? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yesu alizaliwa Betelehemu katika Yudea wakati wa utawala wa mufalme Herode. Kisha kuzaliwa kwake, watu wenye elimu kutoka mashariki wakafika Yerusalema.


‘Ewe Betelehemu, katika inchi ya Yuda, wewe si mudogo kabisa kati ya miji mikubwa ya Yuda, maana ndani yako atatoka mutawala, atakayechunga watu wangu, ndio Waisraeli.’ ”


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Na mashitaki haya yalikuwa yameandikwa juu ya musalaba wake: “Huyu ndiye Mufalme wa Wayuda.”


Maandiko Matakatifu hayakusema kwamba Kristo atazaliwa katika ukoo wa mufalme Daudi na katika muji Betelehemu, pahali Daudi alipoishi?”


Hivyo nikatwaa wale viongozi wenye hekima, akili na ujuzi ambao muliwachagua kutoka katika makabila yenu, nikawaweka kuwa viongozi wenu. Nikawaweka wengine kuwa majemadari wa makundi ya watu elfu moja moja, ya watu mia moja moja, ya watu makumi tano tano na ya watu kumi kumi. Nikachagua vilevile wakubwa wengine wa kuchunga kila kabila.


Kristo alikuwa yuko mbele vitu vyote havijakuwa, na kwa njia ya kuungana naye vyote vinashikamana.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


Tunawaandikia ninyi juu ya Neno la uzima, lililokuwa tangia mwanzo. Sisi tulilisikia, tuliliona kwa macho yetu wenyewe, tuliliangalia na kuligusa kwa mikono yetu wenyewe.


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


“Umwandikie malaika wa kanisa la Smurna hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa wa kwanza na wa mwisho, aliyekuwa amekufa lakini sasa ni muzima.


Akasema tena: “Sasa ni mwisho! Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho. Yule anayesikia kiu, nitamupa maji ya kunywa yanayotoka katika chemichemi ya maji ya uzima pasipo kulipa.


Wakati ule kulikuwa kijana mumoja Mulawi katika muji wa Betelehemu katika inchi ya Yuda.


Hapo zamani, wakati waamuzi walipokuwa wanatawala Waisraeli, kulitokea njaa katika inchi. Mutu mumoja kutoka Betelehemu katika Yuda pamoja na muke wake na watoto wao wanaume wawili walikwenda kuishi kwa muda katika inchi ya Moabu kwa kuishi kama wageni.


Basi wazee waliokuwa kwenye mulango na watu wote waliokuwa pale wakajibu: “Ndiyo, sisi ni washuhuda. Yawe amufanye muke wako akuwe kama Rakeli na Lea, ambao wote wawili waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe upate kustawi katika jamaa ya Efurata, ukuwe na sifa katika Betelehemu.


Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”


Daudi alikuwa mutoto wa Yese, wa ukoo wa Efurata kutoka Betelehemu katika inchi ya Yuda. Yese alikuwa na watoto wanane wa kiume. Wakati Saulo alipokuwa mufalme, yeye alikuwa amekwisha kuwa muzee, mutu mwenye umri mukubwa.


Na yule mukubwa wa kundi la waaskari elfu moja umupelekee siagi hizi kumi. Uwaangalie kaka zako kama wanaendelea vizuri na kisha uniletee habari zao.”


Muchunguze kila upande mujue pahali anapojificha, kisha muniletee habari kamili. Halafu nitakwenda pamoja nanyi na ikiwa angali kule, basi, mimi nitamutafuta kati ya maelfu yote ya watu wa Yuda.”


Atajichagulia wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya waaskari wake wa maelfu na wengine wakuwe wakubwa wa makundi ya watu makumi tano. Atawafanya wengine wamulimie mashamba yake na kuvuna mazao yake. Atawafanya wengine vilevile wamutengenezee silaha za vita, na wengine wamutengenezee vyombo vya magari yake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ