Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Sasa kwa nini munalia kwa sauti? Hamuna mufalme tena? Mushauri wenu ametoweka? Munalalamika kwa uchungu, kama mwanamuke anayezaa!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 4:9
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu watafazaika, watashikwa na hofu na maumivu, watakuwa na uchungu kama mama anapozaa. Wataangalia kwa mashaka, nyuso zao zitaungua kwa haya.


Kwa maono hayo nimeingiwa na woga mukubwa. Maumivu mengi yamenishika, kama maumivu ya mama anayezaa. Nimefazaika zaidi hata siwezi kusikia; nimefazaika hata siwezi kuona.


Kama vile mama mwenye mimba anayezaa analia na kugaagaa kwa uchungu, ndivyo tulivyokuwa kwa sababu yako, ee Yawe.


Enyi wakaaji wote wa Lebanoni, ninyi munaokaa salama kati ya miti ya mierezi, mutaugua sana wakati mutakaposhikwa na uchungu unaokuwa kama wa mwanamuke anayezaa!


Usiogope ee Yakobo, mutumishi wangu, wala usifazaike, ee Israeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Maana nitakuokoa toka huko mbali unapokuwa, nitawaokoa wazao wako kutoka katika uhamisho. Utarudi na kuishi kwa amani, wala hakuna mutu atakayekuogopesha.


Mpaka wakati gani nitaendelea kuona bendera za vita na kusikia mulio wa baragumu?


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Miji yake itatekwa, kuta zake vilevile. Siku hiyo mioyo ya waaskari wa Moabu itakuwa kama vile moyo wa mwanamuke anayezaa.


Mufalme wa Babeli amesikia habari zao. Kwa hiyo, mikono yake ikaregea. Ameshikwa na huzuni na uchungu, kama mama anayezaa.


Sikiliza kilio cha watu wangu, kutoka kila upande katika inchi. Yawe hayuko tena katika Sayuni? Mufalme wa Sayuni hayuko tena? Lakini Yawe anasema: Mbona wamenikasirikisha na sanamu zao za kuchongwa, nayo miungu yao ya kigeni?


Walimunasa yule ambaye maisha yetu yalimutegemea, yule mufalme aliyechaguliwa na Yawe yule ambaye tulisema juu yake: Chini ya ulinzi wake tutaishi kati ya mataifa.


Wakati huo watasema: Hatuna tena mufalme, kwa maana hatumwogopi Yawe; lakini, naye mufalme atatufanyia nini?


Maumivu kama ya kuzaa mutoto yanamufikia. Lakini yeye ni mutoto mupumbafu; wakati wa kuzaliwa unapofika yeye anakataa kutoka ndani ya tumbo la mama!


Hivi ndivyo Waisraeli watakavyokuwa: watakaa kwa muda murefu bila mufalme au mukubwa; bila sadaka, wala nguzo za sanamu wala vyombo walivyotumia kwa kujua mapenzi ya Mungu.


Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.


Wakati mwanamuke anapozaa, anasikia uchungu kwa sababu wakati wake wa kuzaa umetimia. Lakini anapokwisha kuzaa, hakumbuki tena maumivu, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa kwa mutoto.


Mwanamuke yule alikuwa mimba, naye alikuwa akilia kwa sababu ya uchungu na maumivu ya kuzaa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ