Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nawe kilima cha Yerusalema, wewe munara wa Sayuni, ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake, kama muchungaji juu ya kondoo wake, wewe utakuwa tena muji wenye mamlaka sawa zamani. Yerusalema utakuwa tena muji mukubwa wa mufalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 4:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Israeli, ndiye Yakobo, akaendelea na safari yake na kupiga kambi yake ngambo ya munara wa Ederi.


Hata hivyo, mufalme Daudi aliteka kikingio cha Sayuni, ni kusema muji wa Daudi.


Sehemu inayofuata, tokea kwenye pembe ya ukuta na munara wa nyumba ya kifalme ya juu karibu na kiwanja cha walinzi ikajengwa upya na Palali mwana wa Uzayi. Pedaya mwana wa Parosi,


Mufunguke, enyi milango; mufunguke, enyi milango ya tangia zamani, kusudi Mufalme mwenye utukufu aingie.


Sayuni, mulima wa Mungu, unapendeza kwa urefu; muji wa Mufalme mukubwa ni furaha ya ulimwengu.


Ninakulilia kutoka miisho ya dunia, nikikuwa nimevunjika moyo. Uniongoze juu kwenye mulima ambako siwezi kujifikisha.


Shingo yako ni kama munara wa Daudi, uliojengwa kwa kulinda silaha, ambako ngao elfu moja zimetundikwa, zote zikiwa za mashujaa.


Nitakupatia waamuzi wanaokuwa sawa wale wa kwanza na washauri wanaokuwa sawa wale wa zamani. Halafu, Yerusalema utaitwa Muji wa Haki, Muji Mwaminifu.


Leo hii, adui atapiga kambi kule Noba, anainua mukono wake kwa mulima Sayuni, kilima cha Yerusalema.


Alililima vizuri na kuondoa mawe yote, akapanda humo mizabibu bora, alijenga munara wa ulinzi katikati yake, akachimba kikamulio cha divai. Kisha akatazamia lizae zabibu nzuri. Lakini likazaa zabibu chungu.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Lakini watakatifu wa Mungu Mukubwa watapewa ufalme, nao wataupokea ufalme huo milele na milele.


Wakombozi watapanda juu ya mulima Sayuni kwa kuutawala mulima wa wazao wa Esau; naye Yawe atakuwa ndiye Mufalme.


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Enyi wafungwa wenye tumaini, murudi kwenye ukuta wa muji wenu. Sasa mimi ninawatangazia: nitawarudishia mema mara mbili.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Mumoja wa wazao wa Yakobo atatawala naye atawaangamiza watakaobaki katika muji.


“Musikilize mufano mwingine. Mutu mumoja alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha upango, akatengeneza nafasi ya kukamulia matunda ya mizabibu na kujenga munara kwa ajili ya walinzi wa shamba. Kisha kupatana kwa kugawanyana mavuno na walimaji wamoja watakaobaki wakitunza shamba lake, akaenda safari katika inchi ingine.


Kisha Yesu akaanza kusema maneno haya kwa wale wakubwa kwa njia ya mifano: “Mutu mumoja alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha na upango, akatengeneza nafasi ya kukamulia matunda ya mizabibu na kujenga munara kwa ajili ya walinzi wa shamba. Kisha akalipangisha kwa walimaji, akaenda safari katika inchi ingine.


Na kule anatawala juu ya wakubwa wote, wenye mamlaka wote, wenye uwezo wote na wasultani wote na juu ya kila cheo kinachoweza kuwa katika dunia hii na katika dunia itakayokuja.


Hakutakuwa usiku tena, wala hawatakuwa na lazima ya mwangaza wa taa wala jua, kwa sababu Bwana wetu na Mungu wetu mwenyewe atawaangazia, nao watatawala milele na milele.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ