Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mataifa mengine yanafuata njia zao, kwa kuitegemea miungu yao, lakini sisi tunafuata njia zetu kwa kumutegemea Yawe, Mungu wetu, milele na milele.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 4:5
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Lakini mataifa yote katika miji yalimoishi yalijitengenezea miungu yao na kuiweka kwa nafasi zenye kuinuka ambako watu wa Samaria walikuwa wametengeneza.


Hata sasa wanatenda kama vile walivyofanya zamani. Hawamwabudu Yawe, wala hawafuati masharti, maagizo, sheria au amri ambazo yeye Yawe aliwaamuru wana wa Yakobo; ambaye alimupa jina la Israeli.


Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako; tutainua bendera kwa kutukuza jina la Mungu wetu. Yawe akutimizie mapenzi yako yote!


Muangalie kuta zake na kuchunguza pango zake za kukimbilia, mupate kuelezea vizazi vitakavyokuja kwamba:


Nitataja matendo yako makubwa, ee Bwana wangu Yawe; nitatangaza kwamba wewe ndiwe mwenye haki.


Sasa, enyi wazao wa Yakobo, mukuje, tutembee katika mwangaza wa Yawe.


Ee Yawe, Mungu wetu, tulipata kutawaliwa na wabwana wengine ambao si wewe, lakini tunakubali wewe pekee kuwa Mungu wetu.


Katika njia ya maamuzi yako tunakungojea ee Yawe; tamaa yetu ni kulikumbuka jina lako.


Nitafanya nao agano la milele, kwamba sitaacha kuwatendea mema hata kidogo; nitaweka ndani ya mioyo yao utii kwa ajili yangu kusudi wasiniache tena.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Katika siku zilizopita Mungu aliwaachilia watu wa mataifa yote wafuate njia wanazotaka.


Kwa hiyo mutatii sauti ya Yawe, Mungu wenu, mukifuata amri zake na masharti yake ambayo ninawaamuru leo.”


Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ