Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.
Lakini mataifa yote katika miji yalimoishi yalijitengenezea miungu yao na kuiweka kwa nafasi zenye kuinuka ambako watu wa Samaria walikuwa wametengeneza.
Hata sasa wanatenda kama vile walivyofanya zamani. Hawamwabudu Yawe, wala hawafuati masharti, maagizo, sheria au amri ambazo yeye Yawe aliwaamuru wana wa Yakobo; ambaye alimupa jina la Israeli.
Kama hamutaki kumutumikia Yawe, basi muchague leo hii ni nani mutakayemutumikia: kama ni miungu ile ambayo wazee wenu waliitumikia ngambo ya muto Furati, au miungu ya Waamori ambao sasa munaishi katika inchi yao. Lakini mimi na jamaa yangu, tutamutumikia Yawe.”