Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 4:2
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni; utatawala juu ya waadui zako wote.


Heri watu wanaoishi katika ukamilifu, wanaofuata sheria ya Yawe.


Midomo yangu itatangaza sifa zako, maana unanifundisha masharti yako.


Wimbo wa Safari za kidini. Wa Daudi. Nilifurahi waliponiambia: “Twende kwenye nyumba ya Yawe.”


Kila mutu anayemwabudu Yawe, Yawe atamufundisha njia ya kufuata.


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi; sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu. Maana nyumba yangu itaitwa: Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.


Maana kutakuja siku ambapo walinzi watalalamika hivi katika vilima vya Efuraimu: Musimame, tupande kwenda Sayuni kwa Yawe, Mungu wetu.


Yawe, Mungu wako, atuonyeshe njia anayotaka tuifuate, na kile anachotaka tufanye.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Kisha, kila mutu aliyebaki kati ya mataifa yote yaliyokuja kuushambulia Yerusalema, atakuwa akikuja Yerusalema mwaka kwa mwaka, kwa kumwabudu Yawe wa majeshi anayekuwa mufalme, na kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Ataondoa kabisa magari ya vita katika inchi ya Efuraimu, na farasi wa vita kutoka katika Yerusalema; pinde za vita zitatupwa mbali. Naye ataleta amani kati ya mataifa; utawala wake utaenea toka bahari mpaka bahari, toka muto Furati hata miisho ya dunia.


Nao wanafunzi wakaenda kuhubiri fasi zote. Bwana akatumika pamoja nao na kuhakikisha ukweli wa mahubiri yao kwa njia ya vitambulisho walivyofanya.]


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


Imeandikwa hivi katika maandiko ya manabii: ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mutu anayemusikia Baba na kufuata mafundisho yake, anakuja kwangu.


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Lakini mutapokea uwezo wakati Roho Mutakatifu atakaposhuka juu yenu. Nanyi mutakuwa washuhuda wangu katika Yerusalema, katika Yudea yote na Samaria na hata katika inchi zote za dunia.”


Paulo na Barnaba walipotoka ndani ya ile nyumba ya kuabudia, watu wakawasihi warudie tena kuwaelezea maneno yale yale kwa siku ya Sabato iliyofuata.


kwa njia ya uwezo wa vitambulisho na maajabu, na kwa uwezo wa Roho Mutakatifu. Hivi tokea Yerusalema mpaka kufika katika jimbo la Iliriko nimehubiri fasi zote Habari Njema ya Kristo.


“Hii ndiyo amri, masharti na maagizo ambayo Yawe, Mungu wenu, aliniamuru niwafundishe, kusudi muyatimize katika inchi munayokwenda kuirizi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ