Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini kwa upande wangu, nimejazwa nguvu na roho ya Yawe; nimejaliwa kufuata sheria ya Mungu na kuwa na uwezo niwatangazie wazao wa Yakobo kosa lao, niwaambie Waisraeli zambi yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 3:8
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Niko na maneno mengi sana, roho yangu inanisukuma kusema.


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Amenituma kutangaza mwaka wake wa neema, na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi kusudi niwafariji wote wanaoomboleza.


Na tangu leo, ninakufanya kuwa imara kama muji unaozungukwa na kuta, kama munara wa chuma na kama ukuta mugumu sana wa shaba. Utakuwa na nguvu juu ya inchi yote, juu ya wafalme wa Yuda, wakubwa wake, makuhani wake na watu wake wote.


Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.


Nimejaa hasira ya Yawe nami ninachoka kwa kuizuia. Kwa hiyo Yawe akaniambia: Umwange hasira ile katika barabara juu ya watoto na vilevile juu ya makundi ya vijana; nayo itawaangukia wote, mume na muke, nao wazee na hata wale ambao wamezeeka sana.


Manabii wako wamekuonea maono madanganyifu. Hawakufichua wazi uovu wako kusudi wapate kukurudishia hali yako ya mbele. Lakini walikuonea maono ya uongo na ya kupotosha.


Wewe mwanadamu, ujulishe Yerusalema machukizo yake.


Wewe mwanadamu, uko tayari kuwahukumu watu hawa? Basi, uwahukumu. Uwajulishe mambo wazee wao waliyofanya.


Ewe mwanadamu! Uko tayari kutoa hukumu, kuuhukumu muji huu wa wauaji? Basi, ujulishe machukizo yake yote.


Yawe aliniambia: Wewe mwanadamu! Uko tayari kuwahukumu Ohola na Oholiba? Basi, uwatangazie matendo yao ya kuchukiza!


Basi, Roho akaninyanyua juu na kunipeleka mbali. Yawe alinijaza uwezo wake. Nami nikaenda nikiwa na uchungu na hasira katika roho yangu.


Sasa, ewe mwanadamu, uwaelezee Waisraeli habari za nyumba ya Mungu na wajifunze taswira yake. Wapate haya kutokana na machukizo yao waliyotenda.


kwa maana hakuwafundisha sawa vile walimu wao wa Sheria, lakini kama vile mutu mwenye mamlaka.


Yakobo na ndugu yake Yoane, wote wawili walikuwa wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa jina la Boanerge, maana yake ngurumo ya radi),


Mafundisho yangu na mahubiri yangu hayakutolewa kwa maneno ya werevu na hekima ya kimutu, lakini katika onyesho la uwezo wa Roho wa Mungu,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ