Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.
Mwenye ukoma yeyote atavaa nguo zilizochanika, nywele zake hatazichanuliwa, na mudomo wake wa juu ataufunika na atalalamika akisema: Mimi ni muchafu, mimi ni muchafu.
Siku zinakuja ambapo nitaleta njaa katika inchi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini si njaa ya kukosa chakula wala kiu ya kukosa maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Yawe.
Samweli akamwambia Saulo: “Kwa nini unanisumbua kwa kunipandisha?” Saulo akamujibu: “Mimi nina taabu kubwa! Wafilistini wananishambulia kwa vita, na Mungu ameniachilia. Hanijibu tena kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Ndiyo maana nimekuita unijulishe kitu cha kufanya.”
(Hapo zamani katika Israeli kama mutu akitaka kumwomba Mungu shauri, alisema: “Basi, kuja, kuja tuende kwa mwonaji.” Maana mutu anayeitwa nabii siku hizi hapo zamani aliitwa mwonaji).