Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Munajikulisha kwa nyama ya watu wangu, munawachuna ngozi yao, munaivunjavunja mifupa yao, na kuwakatakata kama nyama ya kupika, kama nyama ya kutia ndani ya chungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 3:3
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe.


Waovu wakinishambulia, na kutaka kuniangamiza, hao wapinzani wangu watajikwaa na kuanguka.


Kuna watu ambao meno yao ni kama upanga, na mataya yao ni kama visu. Wako tayari kuwatafuna wamasikini wa inchi, na wakosefu wanaokuwa kati ya watu!


Yawe anawashitaki wazee na wakubwa wa watu wake: Ninyi ndio mulioliharibu shamba la mizabibu; mali wamasikini walizonyanganywa ziko ndani ya nyumba zenu.


Muna haki gani kuwagandamiza watu wangu, na kuwatendea wamasikini vibaya? –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Wanasema hivi: Wakati wa kujenga nyumba haujakaribia bado. Muji ni kama chungu kikubwa, na sisi ni kama nyama.


Tia humo vipande vya nyama, vipande vizuri vya paja na mabega. Ukijaze vilevile mifupa mizuri.


Musikilize, enyi munaowagandamiza wakosefu na kuwaletea maangamizi wamasikini wa inchi.


Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi: Munawatendea watu wangu kama adui. Munawanyanganya watu watulivu nguo zao; watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi, na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ