Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Lakini ninyi munachukia mazuri na kupenda mabaya. Munawachuna ngozi watu wangu, na kunyofoa nyama juu ya mifupa yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 3:2
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Ahabu alipomwona Elia, akasema: “Ewe adui yangu, umeninasa tena?” Elia akamujibu: “Ndiyo! Nimekunasa, kwa sababu wewe umekusudia kabisa kutenda maovu mbele ya Yawe.


Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.


Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja; hakuna anayetenda mazuri, hakuna hata mumoja.


Watu wanaovunja sheria wanasifu waovu, lakini wanaoshika sheria wanapingana nao.


Muna haki gani kuwagandamiza watu wangu, na kuwatendea wamasikini vibaya? –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Ole kwao wanaosema ubaya ni uzuri na uzuri ni ubaya. Wanasema giza ni mwangaza na mwangaza ni giza. Wanasema kichungu ni kitamu na kitamu ni kichungu.


Munafikiri kwamba munafanya sawa, lakini nitayafichua matendo yenu, nayo miungu yenu haitawafalia kitu.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kweli, muji huu ni chungu, na wale waliouawa ndio nyama. Ninyi lazima mutaondolewa katika muji.


Wakubwa wake wanaokuwa ndani ya muji ni kama imbwa wa pori wanaorarua nyama wao; wanaua kwa kujitajirisha kwa namna isiyokuwa ya haki.


Tia humo vipande vya nyama, vipande vizuri vya paja na mabega. Ukijaze vilevile mifupa mizuri.


Munakunywa maziwa, munavaa nguo za manyoya yao na munawachinja kondoo wanono na kuwakula. Lakini hamuwakulishi hao kondoo.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Lakini Yawe anawaambia ninyi hivi: Munawatendea watu wangu kama adui. Munawanyanganya watu watulivu nguo zao; watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi, na wasiokuwa na mafikiri yoyote ya vita.


Hakuna mutu mwaminifu kwa Mungu aliyebaki katika inchi, hakuna mutu yeyote mwenye usawa kati ya watu. Kila mumoja anavizia kumwanga damu; kila mumoja anamwinda mwenzake kusudi amunase.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Wakubwa wake ni simba wanaonguruma, waamuzi wake ni imbwa wa pori wenye njaa magaribi wasioacha chochote mpaka asubui.


Lakini wanainchi wenzake walimuchukia. Kwa hiyo wakatuma wajumbe kumufuata nyuma waende kusema: ‘Hatutaki mutu huyu kuwa mufalme wetu.’


Halafu wakalalamika kwa nguvu: “Hatutaki mutu huyu! Tunataka utufungulie Baraba!” (Yule Baraba alikuwa munyanganyi.)


Watu wa dunia hawawezi kuwachukia ninyi, lakini wananichukia mimi kwa sababu ninashuhudia kwamba matendo yao ni mabaya.


Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Hawatakuwa na upendo wala huruma. Watakuwa wenye kusingiziana, wasiojizuiza, wakali na wasiopenda mema.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ