Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 2:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yule atakayepasua njia atawatangulia, nanyi mutauvunja mulango wa muji na kutoka inje, mutapita na kutoka inje. Mufalme wenu, atawatangulia; Yawe mwenyewe atawatangulia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 2:13
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, malaika wa Mungu aliyekuwa mbele ya kundi la Waisraeli akaondoka akakaa nyuma yao. Na ule munara wa wingu vilevile ukaondoka mbele ukasimama nyuma yao.


Utayafungua macho ya vipofu, utawafungua wafungwa toka katika kifungo, utawaweka huru wale waliofungwa katika giza.


Yawe anasema hivi: Mimi, kweli mimi, ndiye ninayekufariji. Kwa nini wewe unamwogopa mutu ambaye ni wa kufa, mwanadamu ambaye anatoweka kama majani?


Mara hii hamutatoka kwa haraka, wala hamutaondoka mbiombio! Maana Yawe atawatangulia, Mungu wa Israeli atawalinda nyuma yenu.


Mimi nilimufanya kuwa mukubwa na mutawala wa mataifa kusudi yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Inanipasa kuwakomboa hawa watu kutoka kuzimu; sharti niwaokoe kutoka kifo! Ewe kifo, mapigo yako ni wapi? Ewe kuzimu, kuangamiza kwako ni wapi? Mimi sitawaonea tena huruma!


Watu wa Yuda na Waisraeli wataungana pamoja na kumuchagua mwongozi wao mumoja; nao watastawi katika inchi yao. Hiyo itakuwa siku kubwa ya Yezereheli.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


Sasa musikilize, enyi wakubwa wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa wazao wa Israeli! Ninyi ndio munaopaswa kujua namna ya kufuata sheria ya Mungu.


Hao waliolemewa ndio watakaobaki wazima; hao waliopelekwa katika uhamisho watakuwa taifa lenye nguvu. Yawe atawatawala kwenye mulima Sayuni, tangu wakati ule na hata milele.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Yesu alitangulia kuingia pahali pale kwa ajili yetu. Amekuwa Kuhani Mukubwa hata milele, kwa mufano wa Melkisedeki.


Kisha akawaambia makuhani: “Mutwae Sanduku la Agano, mutangulie nalo mbele ya watu.” Nao wakalitwaa na kutangulia mbele ya watu.


Watapigana vita na Mwana-Kondoo, lakini Mwana-Kondoo pamoja na waaminifu wake aliowaita na kujichagulia atawashinda, kwa sababu yeye ni Bwana wa wabwana na Mufalme wa wafalme.”


Kwa maana Mwana-Kondoo anayekuwa katikati ya kiti cha kifalme, atawachunga na kuwaongoza kwenye chemichemi ya maji ya uzima. Naye Mungu atawapanguza machozi yao yote.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ