Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa, kila kitu kilichochumwa kitateketezwa kwa moto. Nitaharibu sanamu za miungu yake yote. Zililundikwa kutokana na mushahara wa ukahaba, nazo zitatumiwa tena kuwa mushahara wa ukahaba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 1:7
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya sherehe kumalizika, watu wote wa Israeli wakakwenda katika kila muji wa Yuda, wakavunjavunja nguzo za mawe na kukatakata sanamu za Ashera, mungu wa kike, na vilevile wakaharibu mazabahu na pahali pa kuabudia miungu mingine. Wakafanya vile katika inchi yote ya Yuda, Benjamina, Efuraimu na Manase, mpaka walipokwisha kuvimaliza vyote. Kisha Waisraeli wakarudi kwao, kila mutu kwenye urizi wake.


Kisha miaka hiyo makumi saba, Yawe atauazibu muji wa Tiro, nao utarudia kufanya uzinzi kwa kujiuzisha kwa mataifa yote ya dunia.


Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.


Pahali pote munapoishi, miji yenu itakuwa ukiwa na sehemu zenu zinazoinuka za kutambikia zitabomolewa, mazabahu zenu zitabomolewa na kuwa ukiwa, sanamu zenu za miungu zitavunjwa na kuharibiwa. Pahali penu pa kufukizia ubani patabomolewa na chochote mulichofanya kitatoweka.


Nitamuvua nguo abaki uchi mbele ya wapenzi wake, wala hakuna mutu atakayeweza kunizuia.


Nitaiharibu mizabibu yake na tini zake, anayosema ni malipo kutoka kwa wapenzi wake. Nitaifanya ikuwe pori, nao nyama wa pori wataikula.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Nitafanya kitambulisho cha ajabu mbinguni na katika dunia; kutakuwa damu, moto na minara ya moshi.


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


“Mwisraeli yeyote, mwanaume au mwanamuke, hatakuwa hata kidogo kahaba wa kidini.


Kile kitu kiovu, ni kusema yule mwana-ngombe muliyejitengenezea, nilikitwaa, nikakiteketeza ndani ya moto, nikakipondaponda na kukisagasaga, kikakuwa mavumbi laini. Halafu nikayatupa hayo mavumbi kwenye kijito kilichotiririka chini ya mulima huo.


Ni kwa sababu mataifa yote yalileweshwa na divai kali ya uasherati wa muji ule. Wafalme wa dunia wamezini nao, na wachuuzi wa dunia wamejitajirisha kutokana na uwingi wa mali zake.”


Wafalme wa dunia waliozini nao na kujifurahisha pamoja nao wataulilia na kuufanyia kilio wakati watakapoona moshi wa moto utakaouteketeza ukipanda juu.


Lakini, kesho yake asubui walipoamuka, waliona kwamba sanamu ya Dagoni imeanguka uso chini mbele ya Sanduku la Yawe, kichwa, miguu na mikono ya sanamu hiyo, vyote vilikuwa vimekatika, vikakuwa vimelala chini kwenye kizingiti cha mulango. Kiwiliwili cha sanamu ya Dagoni ndicho tu kilikuwa kimebakia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ