Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kwa hiyo, anasema hivi: Muji wa Samaria nitaufanya kuwa mabomoko katika mbuga, shamba ambalo watu watapanda mizabibu. Mawe yaliyoujenga nitayatupa ndani ya bonde, na misingi yake nitaichimbuachimbua.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 1:6
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ikiwa atakimbilia katika muji fulani, basi, watu wote wa Israeli wataleta kamba na kukokotea mawe ya majengo yake mpaka katika bonde, na hakutabaki kitu chochote hata jiwe dogo la muji ule.”


Kwa mwisho wa mwaka wa tatu Waasuria waliuteka muji wa Samaria. Ilikuwa katika mwaka wa sita wa utawala wa Hezekia na vilevile mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea mufalme wa Israeli, muji wa Samaria ulipotekwa.


Katika mwaka wa ine wa utawala wa Hezekia, ambao vilevile ulikuwa mwaka wa saba wa utawala wa Hoshea mwana wa Ela mufalme wa Israeli, Salmanaseri mufalme wa Asuria alishambulia muji wa Samaria na kuuzunguka.


Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani? Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani. Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta kuwa lundo la mabomoko.


Ujumbe wa Mungu juu ya muji wa Damasiki. Damasiki utakoma kuwa muji; utakuwa lundo la mabomoko.


Atabomoa pango za miji ya Moabu yenye kuta ndefu na kuiangusha chini ndani ya mavumbi.


Umeufanya muji kuwa lundo la mawe, muji wenye pango kuwa uharibifu. Nyumba za watu wageni zimetoweka, wala hazitajengwa tena upya.


Utapanda tena mizabibu juu ya milima ya Samaria; walimaji watapanda mbegu na kuyafurahia mazao yake!


Mimi ninapingana nawe, ewe mulima muharibifu, mulima unaoharibu dunia nzima! –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitanyoosha mukono wangu juu yako kwa kukuazibu, nitakuangusha kutoka juu kwenye mawe makubwa na kukufanya kuwa mulima uliochomwa kwa moto.


Babeli itakuwa lundo la mabomoko, itakuwa makao ya mbweha, itakuwa machukizo na kitu cha kuzomewa; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Nami nikauliza: Kuna mutu anayekuwa na hekima apate kueleza mambo haya? Ni nani aliyeongea na Yawe hata aweze kutangaza kwa nini inchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mutu anayepita humo?


Namna gani zahabu yetu ilivyochakaa, zahabu safi kabisa ilivyobadilika! Mawe ya bei kali yamesambazwa kwa barabara zote.


Nitaubomoa kabisa huo ukuta mulioupakaa chokaa, na musingi wake utakuwa wazi. Ukuta huo ukianguka, mutaangamia chini yake. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Ninyi munawagandamiza wazaifu na kuwalipisha kodi ya ngano. Munajijengea nyumba za mawe ya kuchongwa, lakini ninyi hamutaishi humo; munalima bustani nzuri za mizabibu, lakini hamutakunywa divai yake.


Bwana wetu Yawe ameapa kwa nafsi yake: Ninachukizwa sana na kiburi cha wazao wa Yakobo; tena ninachukia nyumba zao nzuri sana. –Ni ujumbe wa Yawe.– Muji wao na vyote vinavyokuwa ndani yake nitavipatia waadui zake.


Basi! Kwa sababu yenu, Sayuni utalimwa kama shamba, Yerusalema lundo la makokoto, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Ulitoka kwenda kuwaokoa watu wako, kumwokoa yule uliyemusimika kwa kumupakaa mafuta. Ulimuponda mutawala wa jamii ya waovu, ukawaangamiza kabisa wafuasi wake.


Lakini Yesu akawaambia: “Munaona haya yote? Kweli ninawaambia: hapa hakutabaki hata jiwe moja juu ya lingine; yote yatabomolewa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ