Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.
Akisimama dunia inatikisika; akiyatupia mataifa jicho, hayo yanatetemeka. Milima ya milele inavunjwavunjwa, vilima vya zamani za kale vinaanguka; ni juu yao kulipokuwa njia zake za kale na kale.
Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.