Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Enyi wakaaji wa Lakisi, mufunge farasi wepesi na magari ya vita. Ninyi mulikuwa mumeiga zambi ya watu wa Sayuni, makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 1:13
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”


Yawe ataitupilia Israeli kwa sababu ya zambi za Yeroboamu ambaye alitenda zambi na kuwasukuma watu wa Israeli vilevile watende zambi.”


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Mupango wa kumwua Amazia ulifanyika Yerusalema. Kwa hiyo akakimbilia Lakisi, lakini waadui walituma watu wa kumwua kule.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma majemadari wakubwa watatu pamoja na kundi kubwa la waaskari kutoka Lakisi kwenda kwa mufalme Hezekia kule Yerusalema. Walisafiri na kufika Yerusalema. Nao walipofika waliingia na kusimama karibu na mufereji wa kisima kinachokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea kiwanja cha mufuaji wa nguo.


Alifuata mwenendo wa wafalme wa Israeli, kama vile jamaa ya Ahabu ilivyofanya, kwa sababu muke wake alikuwa binti ya Ahabu. Akatenda maovu mbele ya Yawe.


Nyuma ya hayo, Saniharibu mufalme wa Asuria, ambaye alikuwa angali anauzunguka muji wa Lakisi akiwa na majeshi yake yote, akawatuma watumishi wake Yerusalema kwa Hezekia mufalme wa Yuda na kwa watu wote wa inchi ya Yuda waliokuwa Yerusalema, akisema:


Unaweza kumufunga mbogo kamba kwa kulima shamba, au akokote jembe la kulima?


Musa akamwuliza Haruni: Walikufanya nini watu hawa hata ukawaingiza katika zambi kubwa hivyo?


Watu wa Madimena wamekimbia, wakaaji wa Gebimu wanatafuta makimbilio.


Kisha mufalme wa Asuria alimutuma jemadari kutoka Lakisi na kundi kubwa kumwendea mufalme Hezekia. Jemadari yule alisimama karibu na mufereji wa birika linalokuwa upande wa juu katika barabara kubwa inayoelekea shamba la wafuaji wa nguo.


Kisha yule jemadari aliposikia kwamba mufalme wa Asuria alikuwa ameondoka Lakisi, aliondoka na kumukuta akishambulia muji wa Libuna.


Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kwamba niliachana na Israeli kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mudanganyifu, hakuogopa; naye vilevile alikwenda na kufanya ukahaba!


wakati waaskari wa mufalme wa Babeli walipokuwa wanaushambulia Yerusalema na vilevile miji ya Lakisi na Azeka, ambayo ilikuwa miji pekee iliyobaki ikizungukwa na kuta.


Kelele la waaskari wapanda-farasi na la wapiga mishale litakaposikilika, watu wote watakimbia. Wamoja wao watakimbilia katika vichaka, wengine watajificha katikati ya mawe. Kila muji utaachwa tupu; hakuna mutu atakayekaa ndani yake.


Dada yake Oholiba aliona jambo hilo, lakini akazidi kupotoka kuliko yeye katika tamaa yake, na uzinzi wake ulikuwa mubaya kuliko wa dada yake.


Haya yote yatatukia kwa sababu ya makosa ya wazao wa Yakobo, kwa sababu ya zambi za wazao wa Israeli. Kosa la Yakobo linaonekana wapi? Katika muji wake mukubwa Samaria! Kosa la Yuda linaonekana wapi? Katika Yerusalema kwenyewe!


Basi, Mufalme Adoni-Zedeki akapeleka ujumbe kwa mufalme Hohamu wa Hebroni, mufalme Piramu wa Yarmuti, mufalme Yafia wa Lakisi na mufalme Debiri wa Eguloni, akawaambia:


Lakini niko na neno hili juu yako: kati yako kuna watu wamoja wanaoshika mafundisho ya Balama. Huyu ndiye aliyemufundisha Balaka kwamba awapime Waisraeli, kusudi wakule vyakula vya kutambikia sanamu za miungu na kufanya uasherati.


Lakini niko na neno hili juu yako: unamuvumilia yule mwanamuke Yezebeli, anayejiita kuwa nabii wa Mungu. Yeye anawapotosha watumishi wangu akiwafundisha kufanya uasherati na kula nyama za kutambikia sanamu za miungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ