Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mika 1:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hili ni neno la Yawe lilomufikia Mika, wa muji wa Moreseti wakati Yotamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya juu ya Samaria na Yerusalema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mika 1:1
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika mwaka wa pili wa utawala wa Peka mwana wa Remalia katika inchi ya Israeli, Yotamu mwana wa Uzia, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala Yuda.


Yawe akamwazibu Azaria, akakuwa na ukoma mpaka alipokufa. Alikaa katika nyumba ya pekee na shuguli zake zote za utawala ziliendeshwa na mwana wake Yotamu.


Katika mwaka wa kumi na saba wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, Ahazi mwana wa Yotamu, mufalme wa Yuda, akaanza kutawala.


Katika mwaka wa tatu wa utawala ya Hoshea mwana wa Ela, mufalme wa Israeli, Hezekia mwana wa Ahazia, mufalme wa Yuda, alianza kutawala.


Ahazi alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi mbili, alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita kule Yerusalema. Yeye, hakufuata mufano muzuri wa Daudi babu yake, lakini alitenda maovu mbele za Yawe,


Hezekia alianza kutawala Yuda akiwa na umri wa miaka makumi mbili na mitano, akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka makumi mbili na tisa. Mama yake aliitwa Abiya binti ya Zakaria.


Haya ni maono Isaya mwana wa Amozi, aliyoyaona juu ya inchi ya Yuda na Yerusalema, katika nyakati za utawala wa wafalme hawa wa Yuda: Ahazi na Hezekia.


Yawe anasema hivi: Sikiliza enyi mbingu, tega sikio ee dunia. Mimi nimewalea watoto wangu na kuwakomalisha, lakini sasa wameniasi!


Katika siku za utawala wa Ahazi mwana wa Yotamu na mujukuu wa Uzia, wa inchi ya Yuda, Resini, mufalme wa Aramu, na Peka mwana wa Remalia, mufalme wa Israeli, walienda kuushambulia Yerusalema, lakini hawakuweza kuunyanganya.


Katika siku Hezekia alipokuwa mufalme wa Yuda, Mika wa Moreseti aliwatangazia watu wote kwamba Yawe wa majeshi alisema hivi: Sayuni utalimiwa kama shamba, Yerusalema utabaki mabomoko, nao mulima wa hekalu utakuwa pori.


Hili ni neno ya Yawe lililomufikia Hosea mwana wa Beri katika siku za utawala wa Uzia, Yotamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi, mufalme wa Israeli.


Ikiwa kweli ninyi Waisraeli ni wazinzi lakini, watu wa Yuda basi wasianguke ndani ya makosa! Musiende pahali patakatifu kule Gilgali, wala musiende kule Nyumba ya Uovu. Wala musiape mukisema: Kama vile Yawe anavyoishi!


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Haya ni maneno ya Amosi, mumoja wa wachungaji wa nyama wa muji wa Tekoa. Mungu alimufunulia Amosi mambo haya yote juu ya inchi ya Israeli miaka miwili mbele ya tetemeko la inchi, wakati Uzia alipokuwa mufalme wa Yuda, na Yeroboamu mwana wa Yoasi alipokuwa mufalme wa Israeli.


Ole kwenu ninyi munaostarehe kule Sayuni, nanyi munaoishi katika usalama kwenye mulima Samaria! Ninyi munaonekana kuwa waongozi wa taifa kubwa, ambao Waisraeli wote wanawategemea.


Haya yote yatatukia kwa sababu ya makosa ya wazao wa Yakobo, kwa sababu ya zambi za wazao wa Israeli. Kosa la Yakobo linaonekana wapi? Katika muji wake mukubwa Samaria! Kosa la Yuda linaonekana wapi? Katika Yerusalema kwenyewe!


Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.


Haya ni maono ambayo nabii Habakuki aliyofunuliwa na Mungu.


Maana hakuna hata ujumbe wowote uliotetewa kwa mapenzi ya kimutu, lakini watu walipasha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mutakatifu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ